SERIKALI
ya Tanzania inashiriki katika Maonyesho ya Kimataifa ya Utalii (FITUR)
yanayofanyika katika ukumbi wa IFEMA mjini Madrid, Uhispania.
Tanzania
inawakilishwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa wenye
kuwakilisha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pia katika Falme ya
Uhispania na Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii Duniani (United
Nations World Tourism Organisation), Bodi ya Utalii Tanzania (TTB),
Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA), Eneo la Hifadhi la Ngorongoro
(NCCA), Mamlaka ya Wanyamapori Tanzania (TAWA) na Mamlaka ya Huduma za
Misitu (TFS).
Lengo
la maonyesho hayo ni kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo katika nchi
washiriki ili kuinua sekta ya utalii.Maonyesho hayo yalifunguliwa jana
tarehe 19 Januari 2022, na Mfalme Felipe VI, ambayo yatahitimishwa
tarehe 24 Januari 2022.
Banda
la Tanzania limekuwa kivutio kwa kutembelewa na wageni wengi ambao
wameonyesha nia ya kutembelea Tanzania bara na visiwani. Maonyesho hayo
yanashirikisha nchi zaidi ya 160 na kuhudhuriwa na mawaziri kadhaa wa
Utalii kutoka nchi mbalimbali duniani.
No comments:
Post a Comment