Na Veronica Simba  - REA
Waziri
 wa Nishati January Makamba amewaelekeza viongozi na wafanyakazi wa 
Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuongeza nguvu katika aina nyingine za 
nishati kama inavyofanyika kwenye umeme.
Alisema
 kuwa REA imeendelea kutekeleza kwa ufanisi mkubwa usambazaji nishati ya
 umeme vijijini hivyo ni vyema pia ikifanya hivyo katika aina nyingine 
za nishati zenye matumizi makubwa zaidi, hususan zinazotumika katika 
kupikia.
Waziri
 Makamba alikuwa akizungumza na wafanyakazi wa REA ili kutoa dira na 
mwelekeo wa Wizara ya Nishati, ikiwa ni mara ya kwanza kukutana nao 
rasmi tangu alipoteuliwa kushika wadhifa huo, takribani siku 100 
zilizopita. Alizungumza na wafanyakazi hao jijini Dodoma, Desemba 20 
mwaka huu.
Alisema
 kuwa wengi wanaitafsiri REA kuhusika na nishati ya umeme pekee kutokana
 na kuweka nguvu nyingi kwenye nishati hiyo, hivyo akasema ni muhimu kwa
 Wakala hiyo kuzipa uzito unaostahili nishati nyinginezo ambazo ni 
jukumu lake pia.
“Kazi
 ya REA ni kubwa zaidi, siyo umeme tu. Mnafanya kazi nzuri sana kwa 
upande wa umeme hivyo toeni uzito unaostahili kwa nishati nyingine zenye
 matumizi makubwa.”
Akitoa
 mfano, Waziri Makamba alieleza kuwa tafiti mbalimbali zinaonesha kuwa 
kwa Tanzania, matumizi makubwa ya nishati yako majumbani. Aidha, 
aliongeza kuwa nishati inayotumika zaidi majumbani hususan katika 
kupikia ni tungamotaka.
Alisema,
 asilimia kubwa ya Watanzania wanaishi vijijini na wanatumia nishati ya 
tungamotaka katika kupikia. “Nataka mfanye mabadiliko kwenye nishati ya 
kupikia maana ndiyo inagusa Watanzania wengi zaidi,” alisisitiza Waziri.
Akifafanua,
 alieleza kuwa pamoja na kupeleka umeme vijijini, haitegemewi kuwa 
wakazi wake watatumia nishati hiyo kupikia hivyo ni jukumu la Wakala 
kufanyia kazi suala hilo.
Sambamba
 na agizo hilo, Waziri Makamba aliitaka REA kuimarisha Kitengo chake cha
 Utafiti na kianze mara moja kufanya tafiti mbalimbali zitakazoleta 
mapinduzi makubwa katika sekta ya nishati, hususan vijijini.
“Mathalani,
 kuna mawazo au fikra gani mpya kuwasaidia Watanzania wapate nishati 
safi ya kupikia? Je, nishati ya kupikia ina mchango gani katika kuongeza
 au kupunguza gharama za maisha? Hizi ni baadhi ya tafiti zinazopaswa 
kufanyika,” alisisitiza Waziri.
Katika
 hatua nyingine, Kiongozi huyo mwenye dhamana na sekta ya nishati 
nchini, alitoa maagizo kuwa wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme 
vijijini, wanapobainika kufanya udanganyifu kwenye miradi hiyo, 
wachukuliwe hatua kali ikiwemo kuondolewa kabisa na wasipewe tena fursa 
ya kufanya kazi hizo.
Vilevile,
 washitakiwe kwa Mamlaka zote husika pamoja na kufanya ufuatiliaji ili 
wasipewe kazi nyingine katika eneo lolote ili iwe fundisho kwao kwa 
kuwaumiza wananchi na kuliingizia hasara Taifa.
Pamoja
 na maelekezo hayo, Waziri aliipongeza REA kwa kazi nzuri ambayo imekuwa
 ikifanya na kuitaka kuongeza juhudi zaidi katika kuwatumikia 
Watanzania.
Alisema
 kuwa Serikali inajivunia utendaji kazi wa REA na kwamba ni mojawapo ya 
Taasisi zinazotegemewa sana hivyo akaiasa isiharibu sifa hiyo.
Awali,
 Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy, akiwasilisha taarifa ya 
utekelezaji wa majukumu kwa Waziri, alieleza kuwa kazi kubwa imefanyika 
ambapo hadi sasa upatikanaji umeme vijijini umefikia asilimia 69.6.
Kwa
 upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Wakili Julius 
Kalolo, akizungumza kwa niaba ya Bodi, alimuhakikishia Waziri kuwa 
maelekezo yote aliyoyatoa yatafanyiwa kazi.
Waziri
 aliahidi kuzitafutia ufumbuzi changamoto zinazowakabili wafanyakazi wa 
REA ikiwemo upandishwaji madaraja na kukaimu nafasi mbalimbali kwa muda 
mrefu, kama alivyowasilisha Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi, Tawi la
 REA, Swalehe Kibwana.
Waziri
 wa Nishati, January Makamba (kulia) akipokea Taarifa ya Utekelezaji wa 
Majukumu ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu 
wa Wakala hiyo, Mhandisi Hassan Saidy. Waziri alizungumza na Wafanyakazi
 wa REA, Desemba 20, 2021 jijini Dodoma. Kulia kwa Waziri ni Mwenyekiti 
wa Bodi ya Nishati Vijijini, Wakili Julius Kalolo na wa kwanza kushoto 
ni Mjumbe wa Bodi, Mhandisi Styden Rwebangira.
Waziri
 wa Nishati, January Makamba akizungumza na wafanyakazi wa Wakala wa 
Nishati Vijijini – REA (hawapo pichani), Desemba 20, 2021 jijini Dodoma.
Mwenyekiti
 wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo akizungumza 
wakati wa kikao cha Waziri wa Nishati, January Makamba na wafanyakazi wa
 Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Desemba 20, 2021 jijini Dodoma.
Mkurugenzi
 Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassan Saidy 
akizungumza wakati wa kikao cha Waziri wa Nishati, January Makamba na 
wafanyakazi wa Wakala hiyo, Desemba 20, 2021 jijini Dodoma.
Mwenyekiti
 wa Chama Cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE), Tawi la Wakala wa
 Nishati Vijijini (REA), Swalehe Kibwana (kushoto) akimkabidhi Waziri wa
 Nishati, January Makamba, Risala aliyoisoma kwa niaba ya wafanyakazi. 
Waziri alizungumza na wafanyakazi wa REA, Desemba 20, 2021 jijini 
Dodoma.
Kamishna
 wa Umeme na Nishati Jadidifu, Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi 
Mramba akizungumza wakati wa kikao cha Waziri wa Nishati, January 
Makamba na wafanyakazi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Desemba 20, 
2021 jijini Dodoma.
Mkurugenzi
 Mkuu wa Wakala  wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy 
(kulia) akimwongoza Waziri wa Nishati, January Makamba (kushoto) 
alipowasili Makao Makuu ya REA, Mtaa wa Makole jijini Dodoma, kuzungumza
 na wafanyakazi, Desemba 20, 2021. Pamoja nao ni Mwenyekiti wa Bodi ya 
Nishati Vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo.
Waziri
 wa Nishati, January Makamba (katikati), akisaini Kitabu cha Wageni, 
alipowasili Makao Makuu ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) jijini 
Dodoma, kuzungumza na wafanyakazi, Desemba 20, 2021.
Wafanyakazi
 wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wakimsikiliza Waziri wa Nishati, 
January Makamba (hayupo pichani), alipokuwa akizungumza nao, Desemba 20,
 2021 jijini Dodoma.
Waziri
 wa Nishati, January Makamba (kushoto) akiongozwa na viongozi wa Wakala 
wa Nishati Vijijini (REA) alipowasili Makao Makuu ya Wakala jijini 
Dodoma, kuzungumza na wafanyakazi, Desemba 20, 2021. Kutoka kushoto ni 
Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo, 
Mkurugenzi Mkuu wa REA Mhandisi Hassan Saidy na Mkurugenzi wa Huduma za 
Ufundi, REA Mhandisi Jones Olotu.
 
No comments:
Post a Comment