*Yataka
wananchi kuendelea kuchukua tahadhari za ugonjwa ,ukaguzi kuanza katika
maeneo mbalimbali ya kutolea huduma kwa wananchi.
Na Chalila Kibuda,Michuzi TV
Serikali
imetoa ufafanuzi wa abiria aliyeripotiwa kuwa na anuwai mpya ya UVIKO
-19 (OMICRON) nchini India na kudaiwa ametokea Tanzania na wito
umetolewa wa kuendelea kuchukua tahadhari za kinga za ugonjwa huo.
Akizungumza
na Waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa Wizara ya
Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Profesa Abel Makubi
amesema kuwa Wizara kupitia Maabara Kuu ya Taifa, imekuwa ikisimamia
upimaji wa ugonjwa wa UVIKO-19 nchini ikiwa ni pamoja na kuangalia
anuwai mpya zinazoshabibishwa na mabadiriko ya mara kwa mara ya kirusi
cha UVIKO-19.
Profesa
Makubi amesema hivi karibuni kumetokea unuwai mpya ijulikanayo kama
Omicron (B.1.1.529) iliyoripotiwa kwa mara ya kwanza Afrika ya Kusini na
Botswana.
Amesema
taarifa ya Desemba 5,2021 iliyoripotiwa na vyombo vya habari vya India
na kuenea katika mitandao ya kijamii na kueleza kuwa India waamegundua
abiria mmoja anayerudi nyumbani (India) mwenye anuwai mpya Omicron
ambaye ametokea Tanzania hata hivyo haijajulikana kama abilia huyu
alitokea Tanzania moja kwa moja au alipita Tanzania kuelekea India na
haijulikania alipita wapi kabla ya kufika India.
Katibu
Mkuu huyo amesema kutokana na taarifa hizo, Wizara ya afya imeanza
kufatilia kupitia vyombo vyetu vya ndani na pia kwa kushirikiana ubalozi
wa Tanzania nchini India ili kubaini ukweli wa jambo hili na baadae
kuchukua hatua stahili.
"Nipende
kuwasihi Wanachi kutokuwa na hofu kutokana na habari hii, bali
tuendelee kuwa watulivu na kutekeleza shughuli za maendeleo huku
tukichukua taadhali zote. Ikiwa pamoja na Kunawa mikono kwa sabuni na
maji tiririka, kuvaa barakoa na kujiepusha na misongamano isiyokuwa ya
lazima na kufuata miongozo mbali mbali inayotolewa na Wizara kupambana
na UVIKO-19"amesema Profesa Makubi
Hata
hivyo amesema Wizara imeendelea kuchukua hatua zaidi za kuepusha nchi
yetu isiingie kwenye mlipuko wa nne kwa kuendelea na upimaji kwenye
mipaka na viwanja vya ndege. Kama taratibu zilivyo nchi zingine watu
wote wanaosafiri kwenda nje ya nchi kwa shughuli mbali mbali hupimwa
UVIKO-19.
Wasafiri
wanaogundulika hawana maambukizi ya UVIKO-19 kwa kutumia kipimo cha
RT-PCR hupewa cheti kuwaruhusu kusafiri na wasafiri wanaogudulika kuwa
na maambukizi huunganishwa na Daktari/Hopsitlai ili waanze matibabu,
kuwa katika uangalizi maalumu na kufatiliwa contacts wake.
Maabara
ya Taifa pia imekuwa ikichunguza mabadiriko ya kirusi (Gene sequencing)
kuangalia uwepo wa anuwahi mbali mbali zinazotokana na mabadiriko ya
UVIKO-19 ikiwemo anuwai mpya ya Omicron.
"Tunaomba
kuwatoa wasi wasi watanzania wote kuwa mpaka sasa hatujabaini anuwahi
mpya ya UVIKO-19 (Omicron) ,tunao uwezo wa kubaini anuawahi hii mpya ya
Omicron na tunaendelea kuzifuatitilia sampuli zote tukibaini uwepo wa
anuwahi mpya tutatoa taarifa.
Aidha
mpaka sasa uchunguzi zaidi ya wanasayamsi duniani unaendelea kujua
anuai hii ya Omicron ina madhara ya kiasi gani kwa mtu anapoambukizwa.
Mpaka sasa taarifa kutoka mataifa yaliyobaini wananchi weny virusi
hivi, wamekuwa na dalili za kiasi na nyepesi bila kuingia
mahututi"amesma
Amesema
Viogozi wote wa Mikoa na Wilaya kuweka na kukagua miundo mbinu hasa
hasa sabuni na maji ya kunawa mikono sehemu za mikusanyiko ili tuwekeze
katika kujikinga na UVIKO-19 bila kusubiri athari kubwa ikiwemo kupoteza
maisha baada ya kupata maambukizi.
Wizara
inawahimiza wananchi kujitokeza kuchanja ili kujikinga na UVIKO-19 na
kuanzia tarehe 07/-10/12/2021 tutakuwa na Kampeni Maalumu za elimu za
kuhamasisha wananchi wengi zaidi wajitokeze kuchanja katika kuadhimisha
miaka 60 ya Uhuru wa nchi yetu. Kampeni hizo zitafanyika katika ngazi za
Mitaa, Masoko, Viwanja vya mipira, Stand za bus/daladala, ,Vyuo na
kweye taasisI mbalimbali.
Hata hivyo alibainisha viongozi wote katika Mikoa, Wilaya,Mitaa na vijiji, tusimamie zoezi hili kwa ufanisi.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto
Profesa Abel Makubi akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na
taarifa ya abiria aliyeripotiwa kuwa na Anuwai mpya ya UVIKO-19
(OMICRON) akitokea Tanzania ,jijini Dar es Salaam.Katibu
Mkuu wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia,Wazee na Watoto
Profesa Abel Makubi akizungumza kwenye maabara ya Taifa namna
wanavyochukua Sampuli na kuzima katika maabara hiyo.
No comments:
Post a Comment