Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata
Mulamula akizungumza baada ya kumalzika kwa mkutano wa nane wa Mawaziri
wa Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC
Na Mwandishi wetu, Dakar
Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata
Mulamula (Mb) amesema mkutano wa Nane wa Mawaziri wa Ushirikiano kati
ya China na Afrika (FOCAC) kimefanyika kwa mafanikio makubwa.
Balozi
Mulamula ametoa kauli hiyo jijini Dakr nchini Senegal baada ya
kumalizika kwa kikao hicho kilichofanyika Novemba 29 na 30 2021 nchini
humo.
Amesema
kikao hicho kimekuwa cha mafanikio kwani kimepitisha maazimio makubwa
na mpango kazi ambao umejikita katika kutekeleza maeneo ya kimkakati
ambayo yakisimamiwa kikamilifu yatazinufaisha nchi za Afrika .
Balozi
Mulamula amesema kauli ya China ya kuzihakikishia nchi za Afrika kuwa
itasaidia kuanzisha viwanda vya kuzalisha chanjo za COVID 19 pamoja na
dawa nyingine ni ya kujivunia na ya kupongezwa.
"Tanzania
imefurahishwa na ahadi hiyo kwani jambo hilo litazifanya nchi za Afrika
kuwa na uwezo wa kuzalisha chanjo na dawa nyingine kwa ajili ya
kuwalinda watu wake na kuacha kutegemea msaada., kauli ya Rais Jinping
ni ya kujivunia na ya lupongezwa,"amesema Balozi Mulamula.
Amesema
kikao kimekuwa na mafanikio zaidi kwani mbali na kuangalia maeneo ya
siku zote ya kuendeleza miundombinu na viwanda, kwa mara ya kwanza
umeangalia jinsi ya kusaidia na kuendeleza wafanyabiashara wadogo na wa
kati.
Amesema
uamuzi wa China kwa kutoa kipaumbele katika eneo la kujenga viwanda vya
kuzalisha dawa na chanjo na kuwawezesha wafanyabiashara wadogo na wa
kati ni wa kupongezwa mno kwani mambo hayo ndiyo ambayo Tanzania
ilitilia mkazo katika taarifa yake na kuongeza kuwa wamefarijika kwamba
Rais Jinping ameahidi kusaidia katika eneo hilo.
“Jambo
hili ni zuri na kubwa sana, ni miongoni mwa maeneo ambayo Tanzania
iliyasemea, eneo hilo ndiko watu wengi walikopata ajira hasa akina mama
na vijana tunaishukuru na kuipongeza China kwa kutoa kipaumbeele katika
eneo hilo”, alisema Mhe. Waziri.
Amesema
kikao hicho pia kimeangalia maeneo ya kujengea uwezo wananchi wa Afrika
katika eneo la ufadhili wa masomo ambalo kwa wakati huu limekwama
kutokana na mlipuko wa virusi vya Covid 19 lakini wameahidi kuendelea
nalo pale hali itakapotengemaa.
Ameongeza
kuwa kikao pia kimeangalia suala la kuendeleza kilimo ili kuwa na
kilimo cha kisasa na kuendeleza miundombinu ya kidijitali hasa nyakati
hizi ambazo ni lazima kujiunganisha kidigitali ili kujikwamua kiuchumi.
Amesema
China imesisitiza na kuweka mkazo katika eneo la kundeleza kilimo ili
kuziwezesha nchi za Afrika kujikwamua na umasikini na wameahidi kutoa
fedha na kuleta wataalamu kwa ajili ya kuendeleza kilimo.
Mkutano
huo wa siku mbili ulijumuisha viongozi na wawakilishi kutoka Bara la
Afrika na China uliangalia jinsi China ilivyotekeleza hatua za
ushirikiano kwa kipindi cha miaka mitatu cha 2018-2021 kwenye maeneo ya
miradi ya kimkakati na ukuzaji wa wigo wa biashara kati ya China na
mataifa ya Afrika.
No comments:
Post a Comment