Mwenyekiti
wa Bodi ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Prof. Henry Mahoo, ameshauri
Menejimenti ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kutengeneza Mfumo wa
kiteknolojia utakaopokea taarifa za kila siku za utekelezaji wa majukumu
ya watumishi kuanzia ngazi ya Wilaya, Mkoa hadi Makao makuu kwa lengo
la kuboresha utendaji kazi wa Tume.
Akizungumza
katika kikao chake na Menejimenti jijini Dodoma Prof, Mahoo amesema,
mfumo huo utamsaidia Mkurugenzi Mkuu, Wakuu wa Idara na Vitengo
kufuatilia utekelezaji wa majukumu ya mtumishi mmoja mmoja na kubaini
mapungufu yaliyopo ama, ubora katika utendaji wake.
“Mfuo
huo utaonyesha majukumu waliyopangiwa watumishi,utekelezaji wake,
sanjari na kubadilishana taarifa baina ya viongozi wa idara na vitengo
na watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji.Mfumo huo pia utasaidia
katika kuboresha eneo la ufuatiliaji na tathmini ya uwajibika wa
Watumishi.”
Aidha
Prof. Mahoo amepongeza juhudi za kutanua eneo la Ofisi kwaajili ya
Wataalam wa Tume na kuongeza kuwa Ofisi hizo zitabakia kuwa Ofisi za
Tume Mkoa wa Dodoma mara ujenzi wa jengo la Ofisi za Makao Makuu
zitakapokamilika katika eneo la Njedengwa mjini Dodoma.
Katika
hatua nyingine Prof. Mahoo ameitaka Idara ya Uendelezaji Miundombinu
kuongeza kasi ya kuifanyia matengenezo Mitambo yote ya Tume inayohitaji
kutengenezwa ili iweze kutumika kibiashara na katika shughuli za
ukarabati na ujenzi wa Miundombinu ya Umwagiliaji.
Ameishauri
Idara hiyo kuboresha eneo la maegesho ya Mitambo pamoja na Stoo ya
kuhifadhia vipuli vya Mashine wakati wa Matengenezo katika karakana ya
Tume.
Mkuu
wa kitengo cha ICT, GEOFREY MWAKIJUNGU (aliyekaa) akimwonyesha
Mwenyekiti wa Bodi ya Tume Prof, Mahoo baadhi ya matukio katika Tovuti
ya Tume.
Mwenyekiti wa Bodi Tume ya Taifa ya Umwagiliaji akikagua
Mtambo aina ya EXCAVATOR katika Ofisi za Tume Mkao Makuu Dodoma.
No comments:
Post a Comment