Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imeandaa kongamano la 12 litakalowakutanisha wataalam hao lengo la kujadili ubunifu wenye suluhisho katika utekelezaji wa Ununuzi na Ugavi kwa kutambua ushindani na mapinduzi ya Viwanda kwa maendeleo ya Jamii.
Akizungumza
Jijini Dar es salaam Kaimu Mkurugenzi Matendaji wa bodi hiyo, Godfred
Mbanyi amesema kongamano hilo linatarajiwa kuanza Novemba 30 hadi
Desemba 03 mwaka 2021 na litafanyika katika kituo cha Kimataifa cha
Mikutano Arusha(AICC). Hivyo kawaasa waalikwa wa kongamano hilo kwenda
na wakati ili kuongeza ufanisi katika kongamano hilo.
Mbanyi
amesema katika Kongamano hilo Wataalamu hao watapata nafasi ya
kujadili, kuchambua, kuweka mikakati ya uboreshaji katika Sekta ya
Ununuzi na Ugavi katika Ununuzi wa Umma na Kampuni Binafsi inayoendana
na Sekta ya viwanda ili kuweza kuongeza ajira kwa wananchi hasa kwa
wenye fani ya Ununuzi na Ugavi.
“Mgeni
rasmi katika ufunguzi wa Kongamano la 12 la Wataalamu wa Ununuzi na
Ugavi anatarajiwa kuwa Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba.
''Nawaomba
sana wataalamu, wadau na watu wote wenye nia ya kutambua mchango wa
fani hii katika maendeleo ya Viwanda wajitokeze pale Arusha kuanzia
terehe 30 Novemba mwaka huu” alisema Mbanyi
Amesema
Bodi hiyo imeandaa wataalamu katika mada mbalimbali watakaochanganya
nadharia na vitendo kwa washiriki watakaokuwa kwenye kongamano ili
waweze kupta mapana katika masuala ya Ununuzi na Ugavi kwa namna gani
yanaweza kuchangia mapinduzi ya Viwanda na hatimae kuleta maendeleo
katika nchi.
“Watu
wote wanaotaka kushiriki Kongamano hili wafuate maelekezo yaliyowekwa
kwenye Tovuti ya Bodi hiyo pamoja na mitandao ya kijamii ya Bodi na pia
waakikishe wamefanya malipo yao mapema kabla ya Novemba 30 mwaka huu ili
kuondoa usumbufu wakati wa Kongamano hilo”. Alisema Mbanyi
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB) Godfred Mbanyi akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Kongamano la 12 la wataalamu wa Ununuzi na Ugavi litakalowakutanisha wataalam hao kwa lengo la kujadili ubunifu wenye suluhisho katika utekelezaji wa Ununuzi na Ugavi kwa kutambua ushindani na mapinduzi ya Viwanda kwa maendeleo ya Jamii litakalofanyika jijini Arusha kuanzia Novemba 30 hadi Desemba 03, 2021.
Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB)
Godfred Mbanyi(katikati aliyekaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na
wafanyakazi wa Bodi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto
aliyekaa ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa PSPTB, Paul
Bilabaye(kushoto) pamoja na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya
Taaluma wa Bodi ya wataalamu wa ununuzi na ugavi nchini Tanzania(PSPTB),
Amos Mang’ombe.
No comments:
Post a Comment