HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 20, 2021

OCODE YAIBUKA NA NEEMA KWA SHULE YA MSINGI KIBWEGELE YAKABIDHI DARASA JIPYA KWA DC UBUNGO

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Herry James akizungumza Jambo wakati wa halfa hiyo ya makabidhiano wa chumba cha darasa la awali.NA VICTOR MASANGU

KATIKA kuendelea kuunnga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita katika kuboresha sekta ya elimu kuanzia ngazi za msingi hadi sekondari hapa nchini Shirika la kitaifa lisilokuwa la kiserikali la Organization for Community Development (OCODE) limefanikiwa kujenda chumba kimoja cha darasa la awali katika shule ya msingi Malamba mawili ambalo limegharimu kiasi cha shilingi milioni 27.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Shirika hilo la Ocode Joseph Jackson wakati wa sherehe za makabidhiano ya chumba hicho cha darasa la awali ambapo iliambatana na halfa ya kuwakabidhi tuzo kwa walimu bora wanne ambao wameweza kujituma na kufanikiwa kufanya vizuri katika ufundishaji na ujifunzaji.

Katika halfa hiyo ambayo imefanyika katika viwanja vya shule ya msingi Malamba mawili mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Wilaya ya Ubungo na kuhudhuliwa na viongozi mbali mbali wa serikali, walimu wakuu kutoka baadhi ya shule zilizopo katika manispaa ya ubungo sambamba na maafisa elimu wa shule za msingi na wanafunzi.

Mkurugenzi huyo katika Hotuba yake kwa mgeni rasmi alibainisha kwamab shirika hilo lilianzishwa tangu mwaka 1999 na kupata usajili wake mnamo mwaka 2003 na kwamba linafanya kazi zake kwa ajili ya kuisaidia jamii pamoja na kuboresha maisha ya watanzania ambao wanaishi katika hali duni na wale wenye mahitaji maalumu.

Alisema kwamba wameamua kujenga chumba hicho cha darasa moja kwa ajili ya wanafunzi wa awali kwa lengo la kuweza kuwasaidia katika kupata elimu bora na kwamba shirika lao tangu mwaka 2019 hadi mwaka huu tayari limefanikiwa kusaidia katika sekta ya elimu kwa shule mbali mbali ikiwemo kujenga madarasa mawili katika shule ya msingi Kibwegere, pamoja na Goba na kwamba jumla yanakuwa madarasa matatu.

Pamoja na ujenzi wa madarasa hayo Mkurugenzi huyo alibainisha kuwa katika madarasa hayo wameweza kuweka mdawati yapatayo 30 katika kila shule ulipopita mradi huo, ikiwemo viti 12 pamoja na kupeleka meza tatu katika shule ya msingi Malambamawili.

“Kwa kweli shirika letu la Ocode katika mradi huu ambao tunauendesha katika manispaa ya Ubungo tumeweza kushirikiana bega kwa began a idara ya elimu na uongozi wa manispaa ya Ubungo kwa kweli wanatupa sapoti kubwa na licha ya hayo yote tumeweza kutoa mafunzo mbali mbali kwa walimu wetu wa shule za awali,pamoja na wale wanaofundisha darasa la kwanza hadi la tatu lengo ikiwa ni kuboresha mbinu za ufundishaji zaidi,”alifafanua Mkurugenzi huyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Herry James ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika halfa hiyo ameupongeza uongozi wa shirika la Ocode kwa kuweza kutoa mchango wake wa kuboresha sekta ya elimu pamoja na kuona umuhimu wa kuwathamini na kuwajali watoto wenye ulemavu kwa kuwatengenezea miundombinu ambayo ni rafiki.

“Jamani hawa walimu inatakiwa tuangalie jinsi ya kuishi na hawa walimu maana ni watu muhimu sana katika taifa letu hili la Tanzania, maana wakija kuamua kufundisha mambo ambayo sio mazuri hivyo siis kama serikali tutahakikisha jambo hli la walimu tunaliztilia mkazo ili waweze kufundisha kwa weledi ambao unastahili, “alifafanua mkuu huyo wa Wilaya.

Aliongeza kuwa wao kama serikali watahakikisha kwamba wanaendelea kuboresha zaidi mazingira ya walimu kwa kuwalinda na kuwajengea misingi bora ambayo itawasaidia katika utekelezaji wa majukumu yao ya kuwafundisha wanafunzi na kuhakikisha wanatoa malezi mazuri ambayo yatakuwa ni msaada wa kulisaidia Taifa katika siku za mbeleni.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya alisema kwamba ataendelea kushirikiana bega kwa began a shirika hilo la Ocode kwa kazi zote ambazo zinazifanya katika Nyanja mbali mabli na kuwahimza kuendelea kushirikiana na serikali katika kila jambo kwa manufaa ya wananchi ya kuleta chachu ya maendeleo kwa ujumla.

Kwa upande wake Afisa elimu msingi katika Manispaa ya Ubungo Abdul Buhety alibainisha kwamba ujenzi wa chumba hicho cha darasa la awali katika shule ya msingi Malamba mawili kutaweza kuwa ni mkombozi mkubwa kwa wanafunzi kuweza kupata fursa ya kupata elimu na kujifunza mambo mbali mbali.

“Idadi ya wanafunzi kila mwaka inazidi kuongezeka nah ii yote ni kutokana na kuwepo kwa elimu bila malipo kwa hiyo uwepo wa ujenzi huu wa darasa la watoto wetu ngazi ya awali amabalo limejengwa na shirika la Ocode kwetu sisi ni hatua nzuri ya kuwasaidia watoto wetu wawez e kusoma katika mazingira ambayo ni rafiki kwa hiyo tuwapongeze sana wenzetu kwa juhudi za kuboresha sekta ya elimu,”alisema.

SHIRIKA la kitaifa lisilokuwa la kiserikali la Organization for Community Devolopment tangu kuanzishwa kwake rasmi manamo mwaka 1999 limeweza kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo ya kuisaidia jamii katika Nyanja mbali mbali hususan katika sekta ya elimu ambapo imejenga madarasa, pamoja na kusaidia madaati,viti pamoja na meza za walimu shule mbali mbali.
Mkuu wa Wilaya ya Ubunge Herry James wa kulia akimkabidhi tuzo mmoja wa walimu ambao wameweza kufanya vizuri katika mambo mbali mbali ikiwemo ufundishaji sambamba na ujifunzaji.
Afisa elimu msingi katika Manispaa yay a Ubungo Abdul Buhety akizungumza jambo mara baada ya kukabidhiwa mradi wa darasa hilo la awali kutoka shirika la Ocode.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Malamba mawili wakiwa katika halfa hiyo ya makabidhiano.
Mkurugenzi mtendaji w a Shirika la Ocode Joseph Jackson akifafanua jambo kwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo mara baada ya kukata utepe na kuingia ndani ya darasa la awali kwa ajili ya kujionea jinsi lilivyojengwa.
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Herry James wa kulia akiwa ameshika mkasi kujiandaa na tukio la kukata utepe ikiwa ni ishara ya makabidhiano ya darasa hilo la awali katika shule ya msingi Malambamawili, kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Ocode Joseph Jakson.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad