Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar, Ndg. Salum Mwalimu akifafanua jambo wakati wa
zoezi la uhakiki wa namna chama hicho kinavyotekeleza matakwa ya sheria ya
Vyama vya Siasa na Sheria ya Gharama za Uchaguzi pamoja na kanuni zake mapema
hivi karibuni. Kutoka kushoto ni Mkaguzi Mkuu wa Ndani toka Ofisi ya Msajili wa
Vyama vya Siasa, Bw. Peter Lyimo na Mkuu wa Kitengo cha Usajili wa Vyama vya
Siasa, Bw. Muhidin Mapeyo.Mkaguzi Mkuu wa Ndani
toka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Bw. Peter Lyimo (kushoto) na Mkuu wa
Kitengo cha Usajili wa Vyama vya Siasa, Bw. Muhidin Mapeyo wakikagua orodha ya
viongozi wa Chama cha Demkorasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar wakati wa
zoezi la uhakiki lililofanyika katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu za chama hicho
Zanzabar mapema hivi karibuni.Kaimu Mkuu wa Kitengo
cha Mawasiliano na Elimu ya Uraia wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Bw.
Abuu Kimario na Afisa Sheria, Bi. Grace Mushi wakikagua nyaraka katika moja ya
faili la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wakti wa zoezi wa Uhakiki
wa chama hicho katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu mjini Zanzibar mapema hivi
karibuni.Naibu Katibu Mkuu wa
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar, Ndg. Salum Mwalimu
akionyesha mpango kazi wa chama chake mbele ya watumishi kutoka Ofisi ya
Msajili wa Vyama vya Siasa (hawapo pichani) walipotembelea katika Ofisi Ndogo
za Makao Makuu ya CHADEMA Zanzibar kwa ajili ya zoezi la uhakiki mapema hivi
karibuni.Mkuu wa Kitengo cha
Usajili wa Vyama vya Siasa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa (ORPP), Bw.
Muhidin Mapeyo akiangalia Kadi ya Mwanachama wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA) inayotolewa kwa njia ya Kidigitali walipokuwa katika zoezi
la uhakiki wa vyama vya siasa katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya chama hicho
mjini Zanzibar mapema hivi karibuni.Kutoka kushoto ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha
Mawasiliano na Elimu ya Uraia wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Bw. Abuu
Kimario, Afisa Sheria, Bi. Grace Mushi na Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Ofisi ya
Msajili wa Vyama vya Siasa.
Ujumbe kutoka Ofisi ya
Msajili wa Vyama vya Siasa (ORPP) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya
viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar mara baada ya
kukamilisha zoezi la uhakiki katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CHADEMA
Zanzibar mapema hivi karibuni.(Picha na ORPP)
No comments:
Post a Comment