Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya
Kusimamia, Kudhibiti na Kuratibu Mapato na Matumizi ya Wizara, George
Simbachawene, akizungumza katika kikao cha kupitia taarifa ya Kamati
hiyo kwa robo ya tatu ya Mwaka wa Fedha 2020/2021, kilichofanyika jijini
Dodoma, leo. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Christopher Kadio,
na kulia ni Katibu wa Kamati, Jenitha Ndone.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya
Kusimamia, Kudhibiti na Kuratibu Mapato na Matumizi ya Wizara, George
Simbachawene (kushoto), akiwasili katika ukumbi wa mikutano wa Jeshi la
Zimamoto na Uokoaji kuongoza Kikao cha Kamati hiyo, jijini Dodoma, leo.
Mjumbe
wa Kamati ya Kusimamia, Kudhibiti na Kuratibu Mapato na Matumizi ya
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Utawala na
Rasilimali Watu wa Wizara hiyo, Emmanuel Kayuni, akimfafanulia jambo
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (hayupo pichani),
katika kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika jijini Dodoma, leo.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya
Kusimamia, Kudhibiti na Kuratibu Mapato na Matumizi ya Wizara, George
Simbachawene (wapili kulia), akimsikiliza Mjumbe wa Kamati hiyo,
Kamishna wa Utawala na Fedha wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Mbaraka
Semwanza alipokuwa akifafanua jambo katika Kikao cha kupitia taarifa ya
Kamati hiyo kwa robo ya kwanza na ya tatu ya Mwaka wa Fedha 2020/2021,
kilichofanyika jijini Dodoma, leo. Watatu kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara
hiyo, Christopher Kadio, na kulia ni Katibu wa Kamati, Jenitha Ndone.
Picha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
No comments:
Post a Comment