HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, July 30, 2021

WIZARA YA AFYA YAZINDUA ZOEZI LA USAMBAZAJI CHANJO YA UVIKO 19 JIJINI DAR LEO

 

 Na Humphrey Shao,Michuzi TV Dar es Salaam

 Katibu Mkuu Wizara ya Afya  Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto .Prof. Abel Makubi, amezindua zoezi la  usambazaji wa chanjo  ya UVIKO 19 aina ya Jonson Jonson  Kwenye BOHARI ya Dawa (MSD) iliyopo Keko Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Waandishi wa habari mara baada uzinduzi huo Prof .Makubi  amesema chanjo hizo zitasambazwa  katika mikoa yote 26     ya Tanzania Bara.

"Chanjo hizi ni Bure na zitapatikana katika Hospitali zote zitakazo elekezwa  za Serikali na zile za Binafsi ambazo zitakuwa zimeteuliwa" Amesema Prof Makubi.

Amesisitiza kuwa chanjo hiyo ni Bure na Serikali imesambaza katika mikoa yote kwa idadi tofauti kulingana na visa vilivyoripotiwa katika mkoa huo.

Ametaja kuwa chanjo hii inaanza kutolewa kwa makundi maalum ambayo ni  Wazee ,Watumishi , Watumishi wa majeshi  na Wenye magonjwa hatarishi.

Kwa upande wake Kaimu  Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Dr.Benjamini Hubila amesema mchakato wa usambazaji umekamilika na shirika lake limejipanga vyema kupeleka chanjo hizo kwa wakati.

Amesema MSD itasambaza chanjo hizo ndani ya siku Saba kwa kupitia mtandao wake wa usambazaji dawa nchini

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Prof.Abel Makubi  akionesha  chanjo aina ya Jonson Jonson kwa Wana habari.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Prof.Abel Makubi  akikabidhi  chanjo kwa  Mkurugenzi wa MSD Dr.Benjamini Hubila.
Wafanyakazi wa MSD wakifungua majokofu yanayotumika kuhufadhia chanjo.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Prof.Abel Makubi  akizungumza na Waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa usambazaji wa chanjo ya uviko 19 .
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa MSD nchini, Dr.Benjamini Hubila akitoa ufafanuzi kwa Waandishi wa habari.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad