HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, July 5, 2021

UJUMBE WA KATIBU MKUU CCM DANIEL CHONGOLO BAADA YA KUWASILI VISIWANI ZANZIBAR, SHAKA 'APIGILIA MSUMARI'

 

Mwandishi wetu Zanzibar
 
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi( CCM) Daniel Chongolo amesema Watanzania daima wataendelea kukiamini na kuiunga mkono Chama hicho ambacho ndicho kimebeba dhamana kulinda amani, umoja, mshikamano na  maendeleo endelevu.

Aidha amesema kwa umuhimu huo kamwe hakipoteza muda wa kucheza upatu kwa kuwaunga mkono wasiojua misingi ya Nchi yetu na kwa hilo  watasubiri sana, wakati wao wakiendelea na siasa zao za kubomoa sisi CCM tunaendelea na kasi ya kujenga nchi chini ya uongozi imara wa Rais Samia na Dkt Mwinyi.

Chongolo amyesema hayo wakati akizungumza na wanachama, viongzozi na wakereketwa katika viwanja vya Afisi Kuu ya CCM kisiwandui mara baada ya mapokezi ya sekretarieti ya Halmashauri kuu ya CCM Taifa.

Amewakumbusha  wanasiasa wanaodhani dola au madaraka inaweza kupatikana kwa shari, vurugu, uvunjifu wa amani, uvunjifu wa tunu za Taifa, uzandiki, usaliti dhidi ya nchi kuwa  hilo kamwe halitawezekana kwa vile serikali zinazoongozwa na CCM ziko makini sana.

"Siku za karibuni kumeibuka kikundi cha wanasiasa kinachotokana na waliokataliwa kwenye sanduku la kura na wananchi, sasa wanajipitisha pitisha kila pahala wakilalama, wakieneza chuki, wakiwakebehi viongozi wa nchi, na wakieneza uongo grade A

"Kwa kujishikiza kwenye masuala wanaliyoyaita ni matakwa ya wananchi kumbe ni matakwa yao kwani matakwa ya wananchi yalinadiwa na  ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025, ni vyema wakapumzika maaana hawataambulia chochote katika madai yao," amesema.

 Chongolo alieleza CCM inaridhishwa sana na namna Rais Samia na Mhe Dkt Mwinyi walivyoanza hususani katika kulinda amani, usalama, umoja na mshikamano kwani ndio chachu ya kufanyika kwa maendeleo. Amewataka watanzania waendelee kuiunga mkono serikali ili nchi yetu ipige hatua kimaendeleo.

Awali Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama hicho Shaka Hamdu Shaka amesema katu CCM hakitatelekeza malengo yake ya kisera ya  kutumikia umma au kupuuzia ukosefu wa huduma za kijamii na kuimarisha uchumi nchini  na baadala yake  ikajielekeza katika kubishana na wapigania vyeo na madaraka bila agenda za ustawi wa wananchi.

Amesema CCM inafahamu vita ya kupigania  uhuru imekwisha na   Afrika inajitawala kama ambavyo muasisi wetu Hayati Baba wa taifa Mwalimu Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume waliwahi kutuasa na kutuusia kuwa vita ya kupigania madaraka, wakataja vita hiyo itachochewa na mamluki wa kisiasa kupigania madaraka bila agenda za maendeleo kwa wananchi.

"Niwasihi wanasiasa nchini wajikite kwenye siasa za maendeleo kwa kutoa fikra na mawazo mbadala yanayoweza kuchangia kuboresha ustawi wa wananchi na kuharakisha maendeleo ya nchi yetu. Waachane na siasa za kitoto za kutoa mikwara ya maigizo kwa Rais Samia, wanaoipinga wafanye ukosoaji unaojenga na sio unaobomoa na kutishia kutugawa au kuvunja amani ya nchi," Shaka

Ameongeza katika  kipindi kifupi cha utendaji wa Rais Samia Suluhu Hassan na Rais Husein Ali Mwinyi wameakisi mambo yaliyokuwa yakitamaniwa na jamii yatokee na kufuatwa.  Sauti zao zimetoa mwanga zimewapa matumaini mapya waliokata tamaa na tabasamu akili kutokana na uongozi bora wanaouonesha unaoheshimu taaluma, kusimamia weledi, utawala wa sheria na kutoa maamuzi ya haki.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi( CCM) Daniel Chongolo akisalimiana na viongozi wa Chama hicho baada ya kuwasili katika Afisi Kuu za CCM Kisiwandui visiwani Zanzibar .Chongo ameambatana na viongozi kadhaa wa Chama hicho kutoka Tanzania Bara
Katibu Mkuu wa CCM Daniel Chongolo akiwa na viongozi wa Chama hicho wakiwa na aliyekuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein ambaye wameenda kumsalimia na kupata baraka zake .
 Aliyekuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein(aliyekaa katikati) akimsikiliza Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)Daniel Chongongolo baada ya kufika Afisi Kuu za Chama hicho Kisiwandui  Zanzibar


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad