Atoa Maelekezo mazito kwa DC wa Rungwe.
Alaani watendaji kuvunja Sheria za nchi kwa maslahi yao.
Chama
cha Mapinduzi kimesikitishwa na ongezeko la matatizo ya ujauzito na
utoro yaliokithiri kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari katika
halmashauri ya wilaya ya Rungwe tabia ambayo inachangiwa na vitendo vya
rushwa na urasimu uliokithiri.
Kimebainisha kuwa ni ajabu katika
halmashauri hiyo wamejiwekea utaratibu wa kuwapiga faini wazazi ambao
watoto wao ni watoro au wamepata ujauzito. Kwa wazazi ambao wanafunzi
wao wamepeana ujauzito wanapigwa faini ya shilingi laki mbili na elfu
arobaini na tano kila mmoja.
Vitendo hivyo vimemchefua Katibu wa
Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Ndugu Shaka Hamdu Shaka
wakati akiwa katika mkutano wa Shina 3 Kata ya Kandete, kijiji cha Mwela
Busekelo mkoani hapa na kumuagiza Mkuu wa wilaya ya Rungwe Dkt.
Vincent Anney kusitisha utekelezaji wa uamuzi wa bodi za shule na
kurejeshwa kwa fedha zote zilizokusanywa kama faini kwa waliowapa na
waliopokea (wanafunzi) wa shule za sekondari na msingi.
"Hatuwezi
kukomesha vitendo vya kuwapa mimba watoto wetu wa kike kwa kuendelea
kutozana faini kwa wazazi wote, yaani mtu mwanaye anapewa mimba na pesa
anatozwa (245,000) na mifuko 10 ya saruju pamoja na mtenda kosa hilo
halafu wote wanarejea kwenye jamii" Alisema Shaka
Amefahamisha
kuwa jambo hilo ni kinyume na sheria ya elimu na kwa namna yoyote
haiwezekani kwa waliopewa dhamana ya kuisimamia na kutafsiri sheria
kubadilisha maudhui na kutasiri wanavyotaka wenyewe.
"Maelekezo
ya Chama, mkuu wa Wilaya sitisha utekelezaji wa uamuzi huu kwa shule
zote, na fedha zote zilizokusanywa zirejeshwe kwa wahusika na hatua
stahiki kwa mujibu wa sheria zichukuliwe kwa waliohusika na tupewe
mrejesho ndani ya siku 7." Alisisitiza Shaka.
Shaka amefahamisha
kuwa rushwa na urasimu ni vitendo na tabia ambazo hazitavumiliwa hata
kidogo na CCM na serikali zake katika kuwaletea maendeleo endelevu
wananchi haitutakubali kuona baadhi ya watumishi, watendaji na viongozi
waliokosa uadilifu wanawagombanisha na wananchi watatendaji hao CCM
itaielekeza serikali wapishe mapema ili watanzania wengine wapewe
dhamana hizo kuendeleza gurudumu la maendeleo.
"Niwaombe na nitoe
raia kwa mawaziri, manaibu mawaziri na watendaji wote waliaminiwa na
Rais Samia kumsaidia wanapokuja ziara mikoani washuke hadi vijijni
kusikiliza wananchi kama anavyofanya Waziri Mkuu Majaliwa, huku kuna
shida kubwa wasiridhike na ripoti za mapambio wanazopatiwa, washuke waje
waone uhalisi itawasaidia sana kuwatathmini wasaidizi wao wa ngazi za
chini kama wanakidhi haja ya mbio za kuwaletea wananchi maendeleo"
Amefahamisha Shaka.
Shaka amesema inasikitisha kuona mama mjane
mwenye miaka 67 ambaye binti yake alipewa ujauzito na anapigwa faini
245,000 na mifuko 10 saruji, kinyume na sheria ya elimu huku mkurugenzi,
Tarafa wapo lakini mtendaji wa kata anavunja sheria za nchi wanaeleana
wakati wananchi zaidi kuumia na kuwarudisha nyuma kiuchumi.
"Waliopewa
dhamana lazima mtafisiri kwa usahihi sheria za nchi ili kutoibua kero
zaidi kwa wananchi. Jamii iwalinde watoto ili wakue katika malezi mazuri
na kupata elimu waje kutumikia nchi yao" alisema Shaka.
Hata
hivyo katika katika kikao hicho wananchi walilalamikia utaratibu wa wao
kutakiwa kununua mbolea toka kwenye maduka ya pembejeo ya maafisa ugani
ndio wapewe mbolea iliyotokana na ruzuku ya serikali bila kufanya hivyo
hawapati mbolea ya ruzuku jambo ambalo sio sawa.
Katibu Mkuu wa
CCM Ndugu Daniel Chongolo na Sekretarieti yake ya Halmashauri Kuu ya CCM
Taifa anaendelea na ziara yake mkoani Mbeya.
No comments:
Post a Comment