Na Ahmed Sagaff – MAELEZO
Mkurugenzi
wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa
amewataka maafisa habari za wizara zote kuimarisha mahusiano na
waandishi wa habari ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi.
Msigwa ametoa maelekezo hayo jana jijini Dodoma alipokutana na Wakuu wa
Vitengo vya Mawasiliano Serikalini kutoka Wizara zote kwa lengo la
kujadili masuala mbalimbali namna ya kuboresha vitengo hivyo katika
utoaji wa taarifa za serikali.
“Tafuteni namna nzuri za
kushirikiana na vyombo vya habari, mkiimarisha mahusiano mazuri na
waandishi wa habari, mtafanya kazi zenu kwa urahisi,” ameagiza Msigwa.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi (Mawasiliano Serikalini) wa Idara
hiyo, Zamaradi Kawawa amewataka maafisa hao kuimarisha mahusiano na
wadau wao wote.
“Tuwe na mahusiano mazuri miongoni mwetu, pia baina yetu na watumishi wenzetu wa wizara zetu na wizara nyingine,
Mnamo 2005 Serikali ilianzisha Vitengo vya Mawasiliano Serikalini na
mwaka 2016 Serikali ikapitisha Sheria ya Haki ya Kupata Taarifa ili
wanahabari na wananchi wapate taarifa za utendaji kazi wa Serikali kwa
urahisi.
No comments:
Post a Comment