Na Gift Thadey, Babati
MBUNGE
wa viti maalum (Vyuo vikuu) Dk Pauline Nahato, ametimiza ahadi yake kwa
kukabidhi mapipa 10 ya kuhifadhi takataka kwenye Mji wa Babati Mkoani
Manyara, katika maadhimisho ya wiki ya kutunza mazingira ya ‘Safisha
Kitaa’.
Dk
Nahato amesema ametimiza ahadi aliyoitoa wakati wa ufunguzi wa tamasha
la ‘Safisha Kitaa' aliyoitoa kuwa atakabidhi mapipa 10 ya kuhifadhi
taka, yatakayowekwa kwenye baadhi ya mitaa ya mjini Babati.
Aliwapongeza
wana Babati kwa kuitikia kampeni ya 'Safisha Kitaa' kwani kwa namna
moja au nyingine imefanikisha usafi wa mazingira kwenye baadhi ya mitaa
ya mji huo.
“Kufanya
usafi iwe utamaduni wetu wa kila siku kwani kila mmoja akitimiza wajibu
wake katika kufanya usafi mji wetu wa Babati utazidi kupendeza na
mazingira kuwa mazuri,” amesema Dk Nahato.
Amesema
afya ikiimarika uchumi pia unakua hivyo usafi ni msingi wa afya wa kila
mmoja na mazingira yakiwa safi magonjwa yanakuwa mbali na jamii
inayowazunguka.
Mkurugenzi
wa Mji wa Babati, Fortunatus Fwema akizungumza kwa niaba ya mgeni rasmi
Mkuu wa mkoa wa Manyara, Charles Makongoro Nyerere, amewapongeza
waandaji wa tamasha hilo.
"Pamoja
na kusafisha mazingira kupitia kauli mbiu ya 'Safisha Kitaa' tumeona
vijana wakifanya mazoezi kupitia michezo mbalimbali iliyochezwa,"
amesema Fwema.
Kada
maarufu wa CCM wa mkoa wa Manyara, Cosmas Masauda, amesema Dk Nahato ni
mzalendo wa mji wa Babati kutokea eneo la Bonga hivyo wanampongeza kwa
hatua hiyo.
"Dk
Nahato amedhihirisha msemo wa nyumbani ni nyumbani kwa kitendo chake
cha kununua mapipa 10 ya kuhifadhi taka na kugawa maeneo mbalimbali ya
mitaa ya Babati," amesema Masauda.
No comments:
Post a Comment