HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, July 1, 2021

Gf TRUCKS YAWATAKA WAKANDARASI KUCHANGAMKIA OFFA YA SABASABA


Kampuni ya Gf Trucks & Equipment’s Ltd ya jijini Dar es Salam imewataka wadau wa sekta ya Ujenzi ,Wakandarasi ,Mainjinia na wadau wa madini pamoja na wafanyabiasharara sekta ya usafirishaji nchini kuchangamkia punguzo la bei kwa mashine na magari (trucks )yanayouzwa na kampuni hiyo ndani ya viwanja vya sabasaba


Akizungumza na wandishi wa habari waliotembelea waliotembelea Banda lao ndani ya viwanja vya Maonyesho ya 45 ya Biashara ya kimataifa Afisa masoko Mwandamizi wa kampuni ya GF, Lukolo Jumaa alisema kampunin ya GF imeamua kutoa punguzo maa lumu kwa wateja wetu ambao watatembelea banda letu lililopo katika maonyesho ya sabasaba

Akifafanua zaidi punguzo hilo la bei (sabasaba special) limelenga zaidi katika mitambo inayotumika kwa shunguli za ujenzi (XCMG Motor grade) ambapo wakandarasi wazalendo wenye miradi ya ujenzi hii ndio fursa yao kwani mwaka mpya wa seriklali ndio huu na wakandarasi wazalendo nio kipamumbele katika hili

Pia wanunuzi na wadau wakubwa wa mitambo hii ni Makampuni ya Ujenzi,Makandarasi pamoja na wamiliki wa migodini,Pia tuna magari makubwa ya mizigo FAW,HONG YANG (trucks) pamoja na tipper zinazotumika katika shunghuli mbalimbali zikiwepo machimbo ya mchanga na katika baadhi ya halmashauri zimekuwa zikitumiwa kwa kukusanyia takata na shughuli nyingine.

Akienda mbali zaidi Lukolo alitanabaisha magari hayo ya FAW na HONG YANG Kwa sasa yaliotengenezwa na kiwanda cha GFA kinachomilikiwa na watanzania kilichopo Kibaha mkoani Pwani hivyo katika maonyesho ya mwaka huu tunajivunia kuonyesha magari yaliotengenezwa na wataalamu wetu wakishitikiana na wataalamu kutoka nje

Wakazi Wa jiji la Dar es Salaam wakipita katika banga la kampuni ya GF Trucks Ltd ndani ya viwanja vya maonyesho ya 45 ya Biashara ya kimataifa kuangalia magari yanyotengenezwa na kiwanda hicho kilichopo Kibaha mkoani Pwani




 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad