Na Amiri Kilagalila, Njombe
KUTOKANA
na mapungufu yanayojitokeza katika zoezi la utoaji wa leseni kwa
wafanyabiashara,wakala wa usajili wa biashara na leseni (BRELA) umetoa
elimu ya sheria ya leseni za biashara kwa maafisa biashara wa mikoa
mitatu ya nyanda za juu kusini.
Akizungumza na waandishi wa
habari mara baada ya semina ya siku ya tatu kwa maafisa hao inayoendelea
mkoani Njombe,afisa kutoka kitengo cha leseni katika BRELA Rajab
Chambenga amesema,mchanganyiko wa utoaji wa leseni baina ya BRELA na
halmashauri umesababisha maeneo mengi ada kutozwa tofauti na ana ya
biashara.
Hata hivyo duru zinaarifu kuwapo kwa baadhi ya
wafanyabiashara nchini wanaofunga biashara zao bila mamlaka ya toaji
leseni kujua hatua inayowalazimu wakala wa usajili wa biashara na leseni
kuendeleza zoezi la ukaguzi na utoaji elimu.
Aidha Chambenga
anakiri kuwapo kwa Baadhi ya wafanyabiashara nchini wanaofunga biashara
zao bila taarifa kuwafikia jambo linalowapa wakati mgumu pindi
wanapotaka kuhuisha biashara .
"Baada ya kufanya zoezi la ukaguzi
katika mikoa tofauti tumegundua leseni za kundi 'A' ambazo huwa
zinatolewa na BRELA na kundi 'B' ambazo huwa zinatolewa na
halmashauri,kulikuwa na mkanganyiko ambapo baadhi ya leseni ilitakiwa
zitoke BRELA ikawa inatolewa na halmashauri,na kutokana na hilo hata ada
ambazo zilikuwa zikitozwa haziendani na ile biashara.Kutokana na
changamoto hiyo tukaona ni vema kutoa mafunzo ya sheria za leseni za
biashara kwa maafisa biashara ili kuepukana na hiyo changamoto"alisema
Rajab Chambenga
Baadhi ya Maofisa Biashara kutoka halmashauri
mikoa mitatu ya Njombe,Iringa na Ruvuma akiwemo Majaliwa Hamis Kassim na
Msafiri Mtandi wanasema elimu wanayopatiwa Inawaongezea maarifa ya
kwenda kuwaelimisha wafanyabiashara katika maeneo yao na kwamba baadhi
yao wamekuwa wakishindwa kutambua umuhimu wa kumiliki leseni katika
biashara zao.
"Kukutana kwetu na kupewa mafunzo ya pamoja
tunaamini tutaenda kuboresha utoaji wa leseni kwa wafanyabiashara wetu
na kikubwa tuelewe uchumi wa nchi unajengwa kwa sehemukubwa na
wajasiriamali pamoja na wafanyabiashara na wafannyabaishara ili wafanye
biashara vizuri wanahitaji kupatale leseni"alisema Msafiri Mtandi
Lusietha
Mapunda ni afisa biashara wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa Mkoani
Njombe amesema baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakaidi kujitokeza
kuomba leseni hadi pale wanapopatwa na madhira.
"Niwaombe
wafanyabiashara wajitokeze kuchukua leseni kwa maana kile ni kibali
unapohitaji kufungua biashara,sisi tupo kwa ajili ya kuwalea na
kuwashauri wafanyabiashara katika shughuli zao"alisema Lusietha Mapunda
Mkakati
wa serikali ni kuhakikisha wafanyabiashara wanafanya shughuli zao kwa
mujibu wa sheria pamoja na kupunguza bugudha baina ya wafanyabiashara na
serikali yao.
Abbas
Kotema afisa leseni mwandamizi kutoka BRELA akieleza majukumu ya BRELA
na madhumuni ya semina kwa maafisa ikiwa ni pamoja na kuangali vifungu
vya sheria na njia za kuboresha ili kuwasaidia wafanyabiashara.
Baadhi
ya maafisa biashara wa mikoa mitatu ya nyanda za juu kuini wakiwa
katika semina ya siku ya tatu wakijifunza sheria ya leseni za biashara
ili kufanya kazi na wafanyabisahara katika maeneo yao kwa kufuata
utaratibu na sheria.
No comments:
Post a Comment