HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, April 10, 2021

KANISA LA WASABATO WAADVENTISTA WASHIRIKI IBADA YA PAMOJA NA WATU KUTOKA DINI MBALI MBALI

 


 
Mchungaji wa kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni, Baraka Butoke, akiongea na waandishi wa Habari akielezea dhumuni la ibada hiyo ya pamoja iliyofanyika katika kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni. Leo Jumamosi 10/04/2021, Dar Es Salaam.
 
Mchungaji wa kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni, Baraka Butoke akiongoza ibada kwa maombi, katika kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni. Leo Jumamosi 10/04/2021, Dar Es Salaam.
 
Waimba kwaya wakiimba nyimbo za kumsifu na kumtukuza Mungu, katika kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni. Leo Jumamosi 10/04/2021, Dar Es Salaam.
 
Waumini wakiwa wanasikiliza neno kutoka kwa Mcungaji Baraka Butoke, katika kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni. Leo Jumamosi 10/04/2021, Dar Es Salaam
 
Wageni waalikwa kutoka Maeneo mbali mbali wakiwa wamekaa kujumuika katika ibada ya pamoja, katika kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni. Leo Jumamosi 10/04/2021, Dar Es Salaam.
Wageni waalikwa kutoka Maeneo mbali mbali wakiwa wamekaa kujumuika katika ibada ya pamoja, katika kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni. Leo Jumamosi 10/04/2021, Dar Es Salaam. 
 
********************
Na Mwandishi wetu.
Akizungumza na waandishi wa habari  Mchungaji wa kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni, Baraka Butoke amesema, Leo ni sabato malaamu ambayo kanisa limeamua kujumuika na jamii inayotuzunguka katika kumuabudu Mungu na kula chakula kwa pamoja

Mchungaji Baraka Butoke amesema, Ni sabato ambayo tumealika marafiki zetu majirani zetu na watu ambao wanaoshi katika mazingira magumu hasa ambao sio waimani yetu, ili waje waone tunavyo abudu pia washiliki kula pamoja nasi na Kumsifu Mungu.

Aidha amesema, dhumuni hasa ni kuabudu pamoja na kula chakula pamoja, pia tumefanya mialiko maalumu kwa viongozi wa dini hasa kwenye makanisa na misikiti iliyopo katika eneo hili linalo tuzunguka, na wote kwa pamoja wamejumuika nasi katika iba hii ya leo.
 
"Pia tumealika watoto wanao wanao lelewa katika vituo vya kuleleaa watoto yatima na ambao wapo katika mazingira magumu ili waje washiriki na watoto wetu ili nao wahisi upendo kutoka kanisa hili." Aamesema. 
 
"Hii sio mara ya kwanza sisi kushirikiana na watu mbali mbali katika ibada ya pamoja mfano, kama sabato tatu zilizopita kulikua na kundi maalumu ambalo tulienda kuwatembelea huko walipo na kuwapelekea maitaji mbali mbali, na hii ni programu endelevu tutaendelea kushirikiana nao na kisaidiana nao tunawajenga kimwili lakini pia tunawajenga kiroho." Amesema.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad