Washindi
 wa Pikipiki za miguu mitatu aina ya Lifan Cargo wa Droo ya kwanza ya 
Kampeni ya Weka Pesa na Ushinde ‘Bonge la Mpango’ inayoendeshwa na Benki
 ya NMB, wamekabidhiwa zawadi zao hizo, huku droo ya pili ya promosheni 
hiyo ikiibua washindi wengine 12, wote wakitwaa zawadi zinazofikia 
thamani zaidi ya Sh. Mil. 23.
Hafla
 Kuu ya makabidhiano hayo ilifanyika NMB Tawi la Gongolamboto, ambako 
mkazi wa Kitunda jijini Dar es Salaam, Martha Mmasi, alikabidhiwa 
pikipiki yake na Meneja wa Kanda ya Dar es Salaam, Donatus Richard, huku
 hafla kama hiyo ikifanyika Tukuyu - Mbeya kumkabidhi mshindi mwingine.
Akizungumza
 kabla ya kumkabidhi Martha pikipiki yake, Donatus alibainisha kuwa NMB 
Bonge la Mpango, inalenga kutambua na kuthamini utamaduni chanya wa 
wateja kujiwekea akiba, pamoja na kurejesha kwa wateja wake sehemu ya 
faida ya benki hiyo ya mwaka uliopita, ambako walipata zaidi ya Sh. 
Bilioni 205.
“Wito
 wetu kwa wateja wetu, kuchangamkia zawadi tunazozitowa kupitia NMB 
Bonge la Mpango, ambazo ni pesa taslimu, pikipiki ya miguu mitatu kama 
hii aina ya Lifan, gari dogo ya mizigo aina ya Tata ‘Kirikuu’ na zawadi 
kuu ambayo ni gari ya kifahari aina ya Toyota Fortuner yenye thamani ya 
Sh. Mil. 169”.Alisema Donatus
Wateja
 wa NMB, wanachopaswa kufanya ni kuweka akiba katika akaunti zao kuanzia
 100,000, kiasi ambacho kinaweza kuwa kianzio kwa wateja wapya, ili 
waweze kuwa sehemu ya wateja wanaowania zawadi ya pesa, pikipiki na 
Kirikuu. Pia unapaswa kuwa na akiba ya Sh. Mil. 10 ili kushindania 
Toyota Fortuner.
Kwa
 upande wake, Martha – mfanyabiashara aliyekiri kuathiriwa kibiashara na
 janga la virusi vya corona, lililotikisa toka mwaka jana, alisema 
alikua mwenye furaha isiyo na kifani kwa kuibuka mshindi wa pikipiki 
hiyo, licha ya kufichua kuwa ujio wa Bonge la Mpango ulimsukuma kuongeza
 kasi ya kuweka akiba.
“Kasi
 yangu ya kuweka akiba iliongezeka, nashukuru nikajikuta nashinda na 
kupitia pikipiki hii, ambayo nakiri kuwa nimeshinda kwa bahati yangu na 
sio aina yoyote ya upendeleo, biashara zangu zinaenda kupata nguvu mpya,
 kwani itasaidia kuniingizia kipato na kukuza uchumi wangu,” alisema 
Martha.
Baada
 ya makabidhiano hayo, droo ya pili ilichezeshwa mbele ya Mwakilishi wa 
Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Elibariki Sengasenga, ambapo 
washindi 10 wa zawadi ya pesa taslimu kiasi cha Sh. Mil. 3.3 
walipatikana, sambamba na washindi wengine wawili wa pikipiki aina ya 
Lifan Cargo ambao ni Yusuph Kyando wa Lushoto - Tanga na Rose Mgore wa 
Pamba Road Mwanza - jumla kuu ya thamani ya zawadi zao ikifikia Mil. 23.
Zawadi
 za wiki za Bonge la Mpango ni pesa taslimu na pikipiki 2 za Lifan 
Cargo, wakati zawadi za kila mwezi katika miezi mitatu ya kampeni hiyo 
ni gari dogo la mizigo aina ya 'Kirikuu' na zawadi kuu ikiwa ni Toyota 
Fortuner itakayotolewa mwishoni mwa kampeni hii.
Mshindi
 wa droo ya kwanza ya Kampeni ya  NMB Bonge la Mpango Martha Mmasi 
akionyesha namba za usajili wa Pikipiki ya Miguu mitatu aina ya Lifan 
Cargo baada ya kukabidhiwa na Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam, 
Donatus Richard (wa pili kutoka kushoto) wakati wa hafla iliyofanyika 
katika Tawi la NMB Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam. Kushoto ni 
Meneja wa Tawi la NMB Airport, Restus Assenga na kulia ni Meneja wa Tawi
 la NMB Gongo la Mboto, Demetrius Kagesha.

Mshindi
 wa Droo ya kwanza ya Bonge la Mpango Martha Mmasi akijaribu kuendesha 
Pikipiki ya Miguu mitatu aina ya Lifan Cargo baada ya kukabidhiwa na 
Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaan, Donatus Richard (wa pili kutoka 
kulia) wakati wa hafla iliyofanyika katika Tawi la NMB Gongo la 
Mboto jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Meneja wa tawi la NMB Airport, 
Restus Assenga na kulia ni Meneja wa Tawi la NMB Gongo la Mboto, 
Demetrius Kagesha.
 
 
No comments:
Post a Comment