HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, March 2, 2021

SIWEZI KUKUBALI KUONA RAIS ANASONONEKA KWA WANANCHI KUKOSA MAJI- WAZIRI AWESO

 

Waziri wa Maji Jumaa Aweso amesema hawezi kumuona Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisononeka kwa wananchi wa mijini na Vijijini wakikosa maji.

Hayo ameyasema wakati wa ziara ya kutembelea Viwanda hivyo vya uzalishaji wa mabomba iliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam kwa kutembelea kiwanda cha Simba Pipe na Plasco.

Aweso amewahakikishia Viwanda vya utengenezaji na usambazaji wa mabomba ya maji kuwa changamoto zote zitafanyiwa kazi ili sekta ya maji kufika mbele zaidi kwa kuwa na ushirikiano wa pamoja.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na Viwanda vya Simba na Plasco vyote vinavyozalisha mabomba ya uzalishaji wa mabomba ya kusafirishia maji, Aweso amesema viwanda vya ndani vitaendelea kutoa huduma kwa miradi yote ya serikali kwa usawa.

Amesema, Wizara ya maji inatakiwa kuendeleza mahusiano mazuri na wadau wa sekta ya maji wakishirikiana kwa pamoja na kutakuwa na kikao kikubwa sana baina ya serikali na viwanda vinavyozalisha vifaa vinavyotumika kwenye miradi ya maji.

"Hatutaki kuona viwanda wanashirikiana na vishoka kwani wao ndo wanakwamisha miradi mingi ya maji kukwama na kuwataka watumie njia sahihi ya kupata tenda za usambazaji wa mabomba ya maji kwenye miradi inayoendelea takribani miradi 651," amesema

Aidha, amewataka viwanda hivyo kuanza kutengeneza pampu za kusukumia maji na kulikua na kisingizio kutoka kwa wataalamu kuhusiana na usambazaji wa mabomba kwenye miradi ila amejionea mwenyewe na kusiwe na kisingizio chochote kwa sasa.

Aweso amesema, changamoto ya malipo kwa wakati itafanyiwa kazi kwa sababu wote wanataka kutoa huduma kwa wananchi na watahakikisha malipo yanafanyiwa kwa kazi na kulipwa kwa wakati ili kazi ziweze kuendelea na miradi kukamilika kwa wakati.

Mkurugenzi wa Manunuzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Hellen Lupogo amesema  wamekuwa na ushirikiano mzuri wa viwanda vya uzalishaji mabomba ikiwemo Plasco na Simba Pipe na ziara hii itazidisha mahusiano mazuri Kati ya Mamlaka za maji na viwanda hivi.

Amesema, viwanda hivyo vimekuwa vinafanya kazi zake kwa wakati na hata Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa Mhandisi Cyprian Luhemeja alishatembelea  na kufanya mazungumzo wa viwanda hivi ili kuboresha mahusiano mazuri ya kibiashara.

Naye kwa Upande wa Wakala na Usambazajiw a Maji Vijijini (RUWASA) Mhandisi Clemence Kivegelo amesema kuna changamoto mbalimbali ambazo wameweza kuzipokea kutoka katika Viwanda vya uzalishaji wa mabomba ya kusambazia maji na wameshaanza kuzifanyia kazi.

Amesema, tayari wameshakaa na TRA na Wizara ya Fedha ili kuangalia  msamaha wa kodi (Tax Extansion) kwa viwanda vinavyosambaza mabomba ya kusambazia maji ambapo unaweza kukuta mradi ni wa miaka miwili ila msamaha unatolewa kwa mwezi mmoja

Mkurugenzi Mtendaji wa Simba Pipe  Jitin Pratap Singh amesema wamejipanga katika kuhakikisha wanatoa huduma nzuri kwa wateja wao hususani Mamlaka zote za maji zinazochukua mabomba kutoka kwao wakiwemo RUWASA na DAWASA.

Amesema,  Simba Pipe imeweka mkakati wa kuunda application katika mtandao ili mafundi wanapokuwa kazini kusoma kwa umakini  namna ya kufunga mabomba kwani unapokosea kuunga sehemu moja unakuwa umeharibu mfumo mzima.

"Tunaunga mkono juhudi za serikali za kutimiza adhma ya Rais Dkt John Pombe Magufuli za Tanzania ya Viwanda na Wizara ya maji ya kumtua Mama Ndoo Kichwani," amesema

Aidha, ameongezea na kusema kwa sasa wanazalisha tani 18,000 kwa mwaka kwa mabomba ya HDPE na UPVC na pia ni kiwanda cha kwanza kuzalisha mabomba ya Gesi nchini.

Hata hivyo kwa upande wa kiwanda cha  Afisa Uendeshaji wa Kiwanda cha Plasco, Alimiya Osman amesema wanafurahi kutembelewa na Waziri wa Maji Jumaa Aweso na Uongozi mzima wa RUWASA na DAWASA na wataendelea kushiriana kwa ukaribu zaidi.

Amesema kwa sasa  wanazalisha malighafi za tani 28,000 kwa mwaka na katika tani hizo ni asilimia 70 ni mabomba ya HDPE.

Mkurugenzi Mtendaji wa Sima Pipe Jitin Pratap Sighn akitoa maelezo kwa Waziri wa Maji Jumaa Aweso wakati wa ziara ya kutembelea Viwanda vinavyozalisha mabomba hayo yanayotumika katika miradi mbalimbali ya maji nchini. Waziri aliambatana na Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA Mhandisi Clemence Kivegelo na Mkurugenzi wa Manunuzi DAWASA Hellen Lupogo sambamba na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Godwin Gondwe.
Mkurugenzi wa Manunuzi DAWASA Hellen Lupogo akieleza jambo kwa Waziri wa Maji Jumaa Aweso vinavyozalisha mabomba hayo yanayotumika katika miradi mbalimbali ya maji nchini. Waziri aliambatana na Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA Mhandisi Clemence Kivegele na  Mkuu wa Wilaya ya Temeke Godwin Gondwe.
Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA Mhandisi Clemence Kivegele akielezea namna Viwanda vya Simba Pipe na Plasco vinavyofanya kazi kwa ukaribu mkubwa na Mamlaka za maji kwa ajili ya mabomba yanakusafirisha na kusambaza maji. Waziri Aweso alifanya ziara ya kutembelea viwanda hivyo leo Jijini Dar es Salaam



 




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad