HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, March 16, 2021

RC SINGIDA AZINDUA MAJENGO MATATU SHULE YA MSINGI GEZENARETH

 


Kaimu Afisa Vijana Mkoa wa Singida, Frederick Ndahani (kushoto) akifungua pazia kuashiria uzinduzi wa jengo la Utawala la Shule ya Awali na Msingi ya Genezareth iliyopo Manispaa ya Singida  mwishoni mwa wiki. Kulia ni Meneja wa shule hiyo, Sister Yohana Duwe.

Katibu wa Elimu wa Jimbo Katoliki Singida, Padri Gilbert Mwiru akizungumza katika hafla hiyo.
Kaimu Afisa Vijana Mkoa wa Singida, Frederick Ndahani (kushoto) akitoa zawadi kwa mwalimu mkuu wa shule hiyo.
Wanafunzi wa shule hiyo wakiimba katika hafla hiyo.
Wanafunzi wa shule hiyo wakiimba katika hafla hiyo.
Kaimu Afisa Vijana Mkoa wa Singida, Frederick Ndahani (kushoto) akitoa zawadi.kwa mmoja wa wanafunzi aliyefanya vizuri mtihani wa darasa la nne.
Jengo la chakula lililo zinduliwa.
Jengo la Utawala lililo zinduliwa.
 

Na Dotto Mwaibale, Singida 

KAIMU Afisa Vijana mkoani hapa Frederick Ndahani amewataka walimu na walezi kuwa lea watoto katika maadili ya kizalendo.

Ndahani ambaye alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya  Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Rehema Nchimbi alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki kwenye hafla ya uzinduzi wa majengo matatu ya Shule ya Awali na Msingi ya Genezareth iliyopo nje kidogo ya Manispaa ya Singida.

" Tukiwa na Taifa la wasomi na wazalendo tutaisogeza nchi yetu kwenye uchumi wa juu hivyo ni jukumu la walimu na walezi kuwafundisha watoto wetu maadili ya uzalendo kuanzia shule za awali na kuendelea." alisema Ndahani.

Ndahani alisema anasikitika kuona vijana waliosomeshwa na Serikali ndio wanakuwa mstari wa mbele kupinga mambo ya maendeleo yanayofanyika hapa nchini kutokana na kukosa uzalendo.

Aidha Ndahani alitumia nafasi hiyo kuomba elimu ya kujitegemea ianze kutolewa mashuleni pamoja na kuanzisha miradi itakayo wajenga wanafunzi kiuchumi kuanzia ngazi ya chini. 

Katibu wa Elimu wa Jimbo Katoliki Singida, Padri Gilbert Mwiru aliishikuru Serikali kwa kushirikiana na mashirika ya dini kwa ajili ya kuwaletea maendeleo wananchi  na kueleza kuwa katika Mkoa wa Singida jimbo hilo lina taasisi za elimu 23, shule za msingi 10, Sekondari 8 na vyuo vya kati 5.

Meneja wa shule hiyo ambayo inamikiwa na Jimbo Katoliki Singida, Sister Yohana Duwe  alisema  majengo yaliyozinduliwa ni jengo la Utawala, Bweni na Bwalo la chakula na kuwa ujenzi huo umegharimu zaidi ya Sh.milioni 3000.

Sister Duwe alitumia nafasi hiyo kuiomba Serikali kusaidia kuboresha miundombinu ya umeme na maji ambayo haipo na kueleza kuwa hivi sasa wanatumia umeme wa jua  (sola) pamoja na maji ya mvua ambayo hayakidhi mahitaji. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad