HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, December 19, 2020

Ni Burudani Yenye Viwango Kwenye Ulimwengu wa Soka Wikiendi Hii!

 *EPL na Serie A Kunogesha Wikiendi Ya Mashabiki wa Soka.

NCHINI Uingereza kunako EPL, ligi ndio kwanza inapamba moto! Hapa ni mechi baada ya mechi, waswahili wanasema ‘hatupoi, hatuboi. Timu za EPL zinajambo lao!’

Wikiendi hii ni Man United vs Leeds United, Everton vs Arsenal. Hizi ni mechi zenye historia na burudani ya aina yake. 


Upinzani wa United na Leeds umeanza mwaka 1923 na mara ya mwisho timu hizi kukutana ilikuwa mwaka 2011 ambapo United alimchapa Leeds 3-0. Ni takribani miaka 9 tangu timu hizi zimekutana uwanjani, mengi yametokea ndani ya huo muda na sasa 2020 hii hapa – Leeds United kuwafata Man United pale Old Trafford. Hapatoshi wikiendi hii!!!! 


Upande wa pili ni Everton dhidi ya Arsenal. Timu hizi zilikutana kwa mara ya kwanza mwaka 1905 na mchezo wao wa mwisho walicheza Februari 2020 ambapo Arsenal walishinda 3-2. Japo Arsenal anataabika kwenye EPL huku Everton akiuanza vizuri msimu huu, bado upinzani na uzito wa mchezo huu haujabadilika. Hakika tutaanzia tulipoishia Februari 23, 2020.


Tuvuke mipaka na tutue pale Italia kunako Serie A. Huku tunakutana na michezo miwili ya kukata na shoka wikiendi hii.


AS Roma vs Atalanta, Lazio vs SSC Napoli. Kimeumana Serie A!! 

Roma na Atalanta sio timu za kuzibeza hata kidogo. Kila mmoja anaumwamba wake, japo Atalanta wanaonekana kama ni timu ndogo ila hakuna udogo kwenye ulimwengu wa soka la sasa hivi. Wanauzoefu wa kushiriki mashindano makubwa kama Ligi ya Mabingwa na hivyo mchezo huu utakuwa wa aina yake katika kuwania kinyang’anyiro cha Serie A msimu huu.


Lazio vs Napoli hapa ndio patashika, nguo kuchanika. Hizi ni timu ambazo ni kama zinaendelea zilipoishia msimu uliopita. Wote walikuwa wakiziwania nafasi za juu kwenye msimamo wa Serie A na mchakato ni uleule msimu huu. Dakika 90 kuamua nani mbabe au wote wapo sawa msimu huu?

Mchongo mzima upo kwa Wataalamu wa Meridian, odds za kibingwa kwa michezo hii na mingine mingi ipo hapa.


Jisajili na Meridiabet hapa http://www.meridianbet.co.tz na furaha yako itaanzia hapo. Pakua App ya Meridianbet kwenye simu yako na uanze kubashiri kwa uhuru nyumbani kwako. Pia, unaweza kuweka pesa kwenye akaunti yako kupitia KwikPay, M-PESA au Airtel Money. Kumbuka, daima hauwezi kupoteza tiketi yako ya kwanza ukiwa na Meridianbet, tuna Bonasi ya 100% inakusubiri.


Meridian - Nyumba yenye odds bora na bonasi kubwa!


3 comments:

Post Bottom Ad