Mkuu
wa Mkoa wa Dar es salaam, Aboubakar Kunenge amemuelekeza Mkandarasi wa
Kampuni ya Nyanza inayojenga barabara na Daraja la Kivule kuhakikisha
ifikapo September 30 daraja hilo linakamilika na kuanza kutumika ili
kupunguza kero ya usafiri kwa wananchi.
RC
Kunenge ametoa maelekezo hayo wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi ya
Ujenzi wa miundombinu Wilaya ya Ilala na Temeke ambapo ameonyesha
kuridhishwa na hatua ya ujenzi ilipofikia na kuwataka waongeze juhudi.
Aidha
RC Kunenge amesema ujenzi wa Madaraja hayo unaenda sambamba na ujenzi
wa Barabara ya Kuelekea Hospital ya Wilaya ya Ilala iliyopo Kivule
ambapo amewasisitiza TANROAD na TARURA kusimamia vizuri miradi hiyo na
kuhakikisha inakamilika kwa wakati.
Akiwa
kwenye ukaguzi wa Barabara ya Mbosi RC Kunenge amemuelekeza Mkurugenzi
wa Manispaa ya Temeke kuhakikisha anatoa fedha za kumalizia ujenzi wa
Barabara hiyo ili ikamilike ndani ya mwezi mmoja.
Pamoja
na hayo RC Kunenge amesema tayari amewaelekeza Wakuu wa Wilaya za Mkoa
huo kuhakikisha wanatoka maofisini na kwenda kusikiliza kero za wananchi
pamoja ukaguzi wa miradi ya maendeleo.
No comments:
Post a Comment