HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, August 9, 2020

MWANAFUNZI WA SEKONDARI AANDAA MAONESHO YA WATU WA TANZANIA ILI KUKUZA UTALII, SERIKALI YAMPONGEZA


MWANAFUNZI wa sekondari Rania Nasser (17)ameandaa maonesho ya picha maarufu kama –WATU WA TANZANIA yatakayofanyika ukumbi wa Alliance Francie jijini Dar es Salaam kuanzia Agosti 7 hadi Agosti 12 mwaka huu.

Maonesho hayo yamedhaminiwa na Ubalozi wa Ufaransa kwa siku tano lengo ikiwa ni kusaidia kukuza utalii nchini kutokana na picha hizo kubeba maudhui yanayoonesha shughuli mbalimbali za kiuchumi pamoja na maisha halisi ya mtanzania yaliyojaa simulizi na historia za Taifa letu

Akizindua maonesho hayo rasmi Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Dk.Damas Ndumbaro kwa niaba ya Serikali ya Tanzania aliahidi kuendelea kuimarisha mahusiano ya Kidemokrasia na kiuchumi kati yake na Serikali ya Ufaransa ikiwa ni pamoja na kutumia mahusiano hayo katika kuitangaza Sekta ya utalii iliyopo nchini ili sekta hiyo iweze kutangazika zaidi katika mataifa mbalimbali ulimwenguni.

Amesema “Tanzania na Ufaransa tunamahusiano mazuri kwa muda mrefu hali ambayo kwa kiasi kikubwa inatunufaisha nchi zote kwenye nyanja mbalimbali hivyo ni wajibu wetu kama nchi kuyatunza mahusiano haya ili yanendelee kutunufaisha”.

 Baada ya kuzindua Maonesho hayo Dk.Ndumbaro alipongeza mwanafunzi Rania Nasser kwa jinsi alivyojitoa muda wake na kupiga picha nzuri zinazoonesha uhalisia na jinsi watanzania tunavyoishi kwa upendo Amani na kuamua kuzitoa bure picha zote kwa Bodi ya Utalii Tanzania ili zitumike kukuza utalii nchni.

“Hongera  Rania kwa niaba ya watanzania wote ninakushukuru” amesema  Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje,Dk. Damas Ndumbaro.

Kwa upande wa Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Frederic Clavier, kwa nafasi yake pamoja na mambo mengine ameahidi kuendelea kuzitangaza fursa za utalii zilizopo Tanzania ili sekta hizo ziendeleee kuiamrika na hatimaye kukuza uchumi wa Taifa.

“Sisi Ufaransa tutaendelea kushirikiana na Tanzania ili kila ubunifu unaolenga kuimarisha utalii uweze kuleta maendeleo nchini.” amesema  Balozi wa Ufaransa,Frederic Clavier.

Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania TTB Bi Devotha Mdachi akiahidi kuziweka picha hizo katika vivutio vya utalii nchini na kubanisha kuwa sanaa hii ya picha ambayo imepewa jina la Watu wa TANZANIA wataiendeleza kwa kuwa itasaidia mataifa mengi ulimwenguni kufahamu uhalisia wa maisha ya watanzania vyema na kukuza Utalii

 Naibu Waziri wa Mambo ya nje Dkt Damas Ndumbaro  akiwa na  Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Frederic Clavier, pamoja na Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania TTB Bi Devotha Mdachi wakishirikiana  na Mwanafunzi wa sekondari umri wa miaka 17 Rania Nasser kukata utepe ikiwa ni ishara ya kufungua  maonesho ya picha maarufu kama –WATU WA TANZANIA yaliyoandaliwa na mwanafunzi huyo. Meonesho hayo ya Picha Maarufu kama watu wa Tanzania yatakayofanyika kwa udhamini wa Ubalozi wa ufaransa katika ukumbi wa Alliance Francie kwa siku tano mfululizo kuanzi tareh 7 hadi 12.
  Mwanafunzi wa sekondari umri wa miaka 17 Rania Nasser akimuonesha baadhi ya picha  Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Frederic Clavier
 Mwanafunzi wa sekondari umri wa miaka 17 Rania Nasser akiongea mbele ya wakati wa kuzindua onesho lake la picha alilolipa  jina la –WATU WA TANZANIA linalofanyika katika ukumbi wa Alliance Francie kwa siku tano mfululizo kuanzi tareh 7 hadi 12.
 Naibu Waziri wa Mambo ya nje Dkt Damas Ndumbaro akizungumza kwenye uzinduzi wa maonesho ya picha yaliyopewa jina la –WATU WA TANZANIA yaliyoandaliwa na mwanafunzi Rania Nasser yatakayofanyika katika ukumbi wa Alliance Francie kwa siku tano mfululizo kuanzi tareh 7 hadi 12.

 Naibu Waziri wa Mambo ya nje Dkt Damas Ndumbaro akipokea moja kati ya picha zilizopo kwenye maonesho ya picha yaliyopewa jina la –WATU WA TANZANIA yaliyoandaliwa na mwanafunzi Rania Nasser yatakayofanyika kwa udhamini wa Ubalozi wa ufaransa katika ukumbi wa Alliance Francie kwa siku tano mfululizo kuanzi tareh 7 hadi 12. Watatu kulia ni Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Frederic Clavier, na Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania TTB Bi Devotha Mdachi.

 Naibu Waziri wa Mambo ya nje Dkt Damas Ndumbaro akipokea moja kati ya picha zilizopo kwenye maonesho ya picha yaliyopewa jina la –WATU WA TANZANIA yaliyoandaliwa na mwanafunzi Rania Nasser.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad