HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, July 19, 2020

MGOMBEA URAIS WA ZANZIBAR DKT HUSSEIN MWINYI KWA TIKETI YA CCM APOKELEWA KWA KISHINDI KISIWANI PEMBA


MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi akivishwa shada la maua na kijana wa Chupukizi Zakia Makame na kushoto Mke wa Mgombea Mama Maryam Mwinyi, walipowasili Uwanja wa Ndege Chakechake Pemba leo 19-7-2020, kwa ajili ya kutambulishwa baada ya kuteuliwa kugombea nafasi hiyo kwa Tiketi ya CCM.(Picha na Ikulu)WANACHAMA wa Chama cha Mapinduzi Kisiwani Pemba wakiwa katika barabara ya Chakechake Pemba wakisubiri kumpokea Mgombea wa Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Mhe.Dkt. Hussein Mwinyi, mapokezi hayo yamefanyika leo 19-7-2020 na kufanyika mkutano wa kumpambulisha katika Uwanja wa Kibirinzi Chakechake Pemba.(Picha na Ikulu) MGOMBEA Urais wa Zanzibar kwa Tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Mwinyi akizungumza na Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali alipowasili Uwanja wa Ndege Chakechake Pemba leo 19-7-2020,(Picha na Ikulu)
MGOMBEA Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Mhe.Dkt. Hussein Mwinyi akiwahutubia Wanachama wa CCM na Wananchi Pemba katikia uwanja wa Kibirinzi chakechake wakati wa mkutano wake wa kutambulishwa kwa Wananchi uliofanyika leo katika uwanja huo.(Picha na Ikulu) WANACHAMA wa Chama cha Mapinduzi Kisiwani Pemba wakifuatilia hutuba ya Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi akiwahutubia katika kiwanja cha Kibirinzi Chakechake Pemba wakati wa mkutano wake wa kutambulishwa uliofanyika leo.(Picha na Ikulu) WALIOKUWA Wabunge wa CUF na sasa wamejiunga na Chama Cha Mapinduzi wwakimsikiliza Mgombea wa Urais wa CCM katika mkutano wa kutambulishwa kwa Wananchi kisiwani Pemba uliofanyika katika Uwanja wa Watoto Kibirinzi Chakechake Pemba leo.(Picha na Ikulu)MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar pia Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein akiwasalimia wananchi waliofika katika vuwanja wa Kibirinzi Chakechake Pemba wakati wa mkutano wa mapokezi ya Mgombea Urais wa Zanzibar Mhe.Dkt. Hussein Mwinyi.(Picha na Ikulu)

MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dr. Abdalla Juma Mabodi , alipowasili Uwanja wa Ndege Chakechake Pemba kuhudhuria mkutano mapokezi ya Mgombea Urais wa Zanzibar Mhe.Dkt. Hussein Mwinyi leo,19-7-2020, (Picha na Ikulu)
 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad