HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, January 27, 2020

Tamasha la KAN lamalizika kwa kishindo


Msanii Fareed Kubanda maarufu kama Fid Q akitumbuiza kwenye jukwaa la KAN


Msanii Tear Drops kutoka Kenya akitumbuiza kwenye jukwaa la KAN
Msanii Lawrence Okello kutoka Uganda kwenye siku ya kufunga tamasha la KAN


Mpenzi wa burudani Kazeneza akishangilia kwenye tamaasha la KAN
Umati wa mashabiki kwenye tamasha la KAN siku ya mwisho
Msanii Victor Kunonga na Mwenzake kutoka Zimbabwe wakitumbuiza
Wafanya kazi wa KAN wakimbeba Mkurugenzi waKAN Dave Ojay kushiria furaha siku ya kufunga tamasha.
 
 
Msimu wa pili wa tamasha la Knowldge Art and Networking (KAN) umemalizika jana kwa kishindo na kuacha wapenzi wa burudani wakiwa na hamu ya kuendelea kupata burudani. 

Tamasha hilo lenye kauli mbiu ya Maendeleo ni Watu Si Vitu imetokana na moja ya nukuu za Mwalimu Julius Nyerere lilifanyika kwenye viwanja Chuo cha Maendeleo na Ushirikiano wa Kimataifa (MS TCDC) kuanzia tarehe 22 mpaka 25 Januari mwaka huu. 

Tamasha hili lilikua na fursa za kujifunza kutoka kwa wasanii wa sanaa za maonesho na utumbuizaji kutoka nchi saba za Afrika, kushirikishana maarifa na kuendeleza mahusiano yetu ya karibu katika jukumu letu la kuleta maendeleo, lakini pia kujenga mtandao. 

Tamasha hili pia litahusisha wasanii wanaojikita katika sanaa ya kutoa uelewa wa maarifa mbalimbali (Conscious artists), ikiwa ni pamoja na wasanii wa sanaa za maonesho na utumbuizaji. Sanaa hii hujikita katika kuleta ufahamu na kuzunguzumzia masuala ya maendeleo na urithi wa tamaduni za Kiafrika. Pia wasaani hao watazungumzia masula yanayohusiana na jamii ya mkoa wa Arusha na Afrika kwa ujumla. 

Kwa ujumla, malengo makuu ya tamasha hili ni pamoja na kutoa nafasi kwa wadau wa maendeleo kuakisi yaliyopita wakati wakitafakari yanayokuja, kutazama fursa zilizopo katika taaluma na kuhamasisha.

Pili, tamasha linalenga kutoa fursa kwa ajili ya kuchambua changamoto zilizopo katika jamii kama vile mimba za utotoni, wakimbizi, tatizo la ajira kwa vijana, rushwa, kisha kuchukua hatua za kukabiliana na changamoto hizi. 

Na tatu ni kutengeneza na kuimarisha mtandao wa wadau wa maendeleo na uongozi ambao umeazimia kutoa mwamko kwa jamii ambao utaleta hamasa kwa jamii ya Waafrika. 

Ezra vMbogori ni Mkurugenzi wa MSTCDC alisema,MSTCDC inatambua nguvu ya sanaa na kuamini kwa dhati kuwa kuiambatanisha sanaa pamoja na maisha katika jamii, inaweza kuwa ni njia thabiti ya kuiimarisha jamii. 

"Jitihada za kuboresha hali ya maisha, kupunguza kutokuwepo kwa usawa, ni katika mambo yanahusishwa katika mila na desturi zilizorithiwa katika mfumo wa jamii. Utamaduni, ikiwa ni pamoja na sanaa, ni njia ya kuleta maendeleo ambayo tukijikita nayo inaweza kutuletea maisha mapya katika jamii,"alisema Mbogori.

Wasanii waliotumbuiza kwenye jukwaa la KAN ni pamoja na Vitali Maembe, Fid Q, Siti & The Band, Florence John from Tanzania, Sandra Nankoma kutoka Uganda, Juma Tutu, Bengatronics kutoka Kenya, Victor Kunonga kutoka Zimbabwe, na Isabella Novela kutoka Mozambique. 

Tamasha hilo pia lilileta paamoja wasanii wa kazi za mikono 9 wakiwa na kazi mbalimbali kutoka Nchi tano za Afrika ikiwemo Kenya, Uganda, Tanzania, Congo na Zimbabwe. 

artivists came up with different projects that they will be working between January 8 towards festival date and they will showcase their projects during the project. 

Wasanii hao ni Mugabo Baretigire, Pamela Aobo, Arinitwe Peter, Sikhulile Sibanda from Zimbabwe Masoud Kibwana, Emmanuel Manoti Anderson, Naiteiemu Nyanjom na Reuben Kabamba.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad