·Wateja wa Airtel Money kutuma pesa bila kuhofia makato ya kutolea
Ukitumia AIRTEL MONEY huna haja ya kukotoa gharama za kutolea, Menu
imerahisishwa kukufanyia hayo yote.
Kampuni ya simu za mkononi ya
Airtel Tanzania leo imezindua huduma ambayo ni suluhisho kwa wateja wa
Airtel Money. Huduma hiyo inayojulikana kama ‘Tuma na ya Kutolea’
itakuwa ni suluhisho kwa wateja wa Airtel Money pale wanapotuma hela.
Huduma ya Tuma na ya Kutolea itawawezesha wateja wa Airtel Money
kutuma pesa kwa wapendwa wao, ndugu, marafiki pamoja na wanafamilia
bila kujisumbua kukokotoa gharama ya hela ya Kutolea.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa kuzindua huduma hiyo,
Mkurugenzi wa Airtel Money Isaack Nchunda alisema, ‘Tunazindua huduma
hii ikiwa ni kuadhimisha yale tuliohaidi katika wiki ya huduma kwa
wateja ambapo ilianza tangu Oktoba 7 mwaka huu. Airtel imedhamiria
kuendelea kuhakikisha ya kwamba inatoa huduma bora muda wote na hii
ndio sababu tumekuwa tukiwaletea wateja wetu huduma na bidhaa ambazo
ni za kiwango cha juu kabisa’.
Kwa muda mrefu, tumekuwa tukiona wateja wa Airtel Money wakituma pesa
pamoja na ya ziada ambayo lengo lake ni kufidia gharama za Kutolea
ambazo ni maarufu kama Tuma na ya Kutolea. Sisi Airtel nia yetu ni
kuwapa wateja wetu kilicho bora, leo Airtel imekuja na huduma ambayo
ni suluhishi wakati wa kutuma pesa kwani gharama za Kutolea zitakuwa
zikikatwa wakati wa kutuma kwa kupitia menu ya Airtel Money. Nia yetu
ni kuifanya huduma hii kuwa rahisi, nafuu na ya haraka pale mteja
anapofanya miamala yake,’ Nchunda alisema.
Airtel imekuwa ikizundua na huduma na bidhaa za kipekee ambazo
zinakidhi matakwa ya wateja wetu pamoja na kugusa maisha yao ya kila
siku. Tuma na ya Kutolea ni huduma ya kipekee ambayo inawafanya wateja
wetu kuendelea kufurahia huduma za Airtel Money, Nchunda aliongeza.
Nchunda alisema kuwa huduma hii inapatikana kwa urahisi. Kuanzia sasa,
wateja wa Airtel Money hawatakuwa na hofu yoyote kuhusu gharama za
Kutolea pesa kwani kupitia Tuma na ya Kutolea huduma ya kutuma pesa
sasa imerahisisha kwa kutuma pesa pamoja na ya Kutolea.
Kwa mteja wa Airtel Money kufurahi huduma ya kutuma pamoja ya Kutolea,
atatakiwa kufuata maelekezo yafuatavyo;
· Kupiga menu ya Airtel Money *150*60#
· Changua 1 Tuma Pesa
· Changua 3 Tuna na ya Kutolea
· Changua namba ya Kutuma ya Airtel
· Ingiza namba ya kutuma
· Weka kiasi cha kutuma
· Weka namba yako ya siri
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice
Singano alisema, Airtel inatambua kuwa ni muhimu kuweka mahitaji ya
wateja wetu mbele. Ni kwa kupitia Airtel Money ambapo mteja anaweza
kutuma pesa bure na sasa tumekuja na huduma suluhishi kwenye gharama
za Kutolea. Tunajivunia kuwa na huduma zenye uwazi ambapo kwa sasa
wateja watakuwa na uhakika wa kujua gharama halisi ya kutolea pale
wanapotumia huduma ya Tuma na ya Kutolea. Airtel itaendelea kutoa
huduma ambazo utapatikanaji wake ni rahisi, nafuu na za haraka ili
kukidhi mahitaji ya wateja.
Kwa sasa, Airtel inaendelea kuwekeza kwenye mtandao ili uendelee kuwa
mpana zaidi na kutoa huduma za kifedha bora zaidi hapa nchini.
Airtel sasa inajivunia kuwa na zaidi ya 1,000 Airtel Money branches na
mawakala wa Airtel Money zaidi ya 60,000 ambapo wateja wetu wanaweza
kupata huduma zote za Airtel kama vile kusajili kwa alama ya vidole,
simu mpya za smartphone, vifaa vya simu pamoja huduma nyingine nyingi.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuzindua huduma ya ambayo ni suluhisho kwa wateja wa Airtel Money. Huduma hiyo inayojulikana kama ‘Tuma na ya Kutolea’ itakuwa ni suluhisho kwa wateja wa Airtel Money pale wanapotuma hela na itawawezesha wateja wa Airtel Money kutuma pesa kwa wapendwa wao, ndugu, marafiki pamoja na wanafamilia bila kujisumbua kupiga hesabu za gharama ya hela ya Kutolea.
Mkurugenzi wa Airtel Money Isack Nchunda akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuzindua huduma ya ambayo ni suluhisho kwa wateja wa Airtel Money. Huduma hiyo inayojulikana kama ‘Tuma na ya Kutolea’ itakuwa ni suluhisho kwa wateja wa Airtel Money pale wanapotuma hela na itawawezesha wateja wa Airtel Money kutuma pesa kwa wapendwa wao, ndugu, marafiki pamoja na wanafamilia bila kujisumbua kupiga hesabu za gharama ya hela ya Kutolea.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania na Mkurugenzi wa Airtel Money wa kampuni hiyo Isack Nchunda wakionyesha bango baada ya kuzindua huduma ambayo ni suluhisho kwa wateja wa Airtel Money. Huduma hiyo inayojulikana kama ‘Tuma na ya Kutolea’ itakuwa ni suluhisho kwa wateja wa Airtel Money pale wanapotuma hela na itawawezesha wateja wa Airtel Money kutuma pesa kwa wapendwa wao, ndugu, marafiki pamoja na wanafamilia bila kujisumbua kupiga hesabu za gharama ya hela ya Kutolea.
No comments:
Post a Comment