HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, September 17, 2019

TANESCO WAJIPANGA KUMALIZA KABISA TATIZO LA UKATIKAJI UMEME

Na Woinde Shizza michuzi TV,Arusha

Shirika la umeme Tanzania limesema kuwa limejipanga kuhakikisha adi ifikapo mwaka 2025 tatizo la ukatikaji wa umeme mara kwa mara litakuwa limeisha kabisa na wananchi wao watakuwa wamesahau kabisa shida hiyo.

Hayo yamebainishwa na kaimu Naibu Mkurugenzi  Mtendaji wa shirika la umeme (Tanesco )Muhandisi Raimondi seya wakati akiongea na waandishi wa habari mara bada ya kufunga semina ya kuwajengea uwezo waandisi wa matengenezo,mameneja wa shirika hilo wa mikoa na kanda iliokuwa ikifanyika leo katika ukumbi wa Corridor uliopo ndani ya jiji la Arusha ambapo alisema kuwa nakulikuwa tatizo la kukatika umeme mara kwa mara lakini sasa hivi limepungua kwani wameboresha zaidi katika sehemu mbalimbali na umeme haukatiki tena mara kwa mara.

Alisema kuwa shirika hilo wanataka waendelee kuboresha zaidi kwa viwango vyakimataifa vya umeme ambapo umeme unatakiwa kutokatika kabisa na kama utakatika ukatike mara nne kwa mwaka na mkakati wa kutekeleza hayo umeanza leo katika kikao hicho ambacho wanaamini ni sehemu ya muarubaini wa tatizo hilo ,maana waandisi hawa wametengeneza matatizo na sababu ambazo zinasababisha umeme huu kukatika na wanaanza kuyafanyia kazi.

‘’dhana kamili ya semina hii ni kuhakikisha waandisi hawa wanaa na kuhakikisha moja ya kazi ambayo waandisi hawa watafanya ni kuhakikisha kwamba umeme haukatiki umeme kabisa kwa sababu umeme unavyokatika hata kwa dakika moja ni hasara kubwa sana kwani kwanza kabisa umeme unavyokatika unailetea serikali hasara kwani inakosa pesa,kwa upande wa viwanda vyetu navyo vinapata hasara kwa mfano kiwanda cha kutengeneza plastiki umeme ukikatika gafla kama wanaendelea kuzaliha wanakuwa wameharibu matirio yale waliokuwa wanatengenezea kwa hiyo hii itachangia kufukuza wawekezaji wa viwanda hivyo ndio maana tumekaa tukaaamua kujadli na kuwapa mafunzo ya wiki mbili na tumetoka na makubaliano yakuhakukisha umeme haukatiki ovyo”alisema Seya

Alisema kuwa wanataka kuhakikisha kili mwananchi anapokea na kunufaika na umeme wa uhakika lakini pia katika sera yetu ya Tanzania ya viwanda haiwezi kufanyakazi vizuri kama umeme utakuwa sio wa uhakika ,na pia kama umeme hautakatika mara kwa mara pia tutawavutia wenye viwanda kuja kuwekeza hapa nchini kwetu na wakija kuwekeza serikali yetu itaongeza mapato , na pia ajira zitaungezeka kwa wananchi wetu.

Kwa upande wa muhandisi Mahende Mgaya meneja mwandamizi wa usambazaji wa shirika la umeme Tanzani alisema kuwa alisema wamechukua kumbukumbu za chanzo cha kukatika umeme za kuanzia mwaka 2015 iliopita wakazi chakata na kujua tatizo ninini na baada ya hapo wakatengeneza mkakati ambao wameugawa kwa awamu tatu ambapo awamu ya kwanza wataangalia tatizo,watalifanyia tatizo na mwisho wataakikisha tatizo limeisha kabisa.

‘lengo letu ninini kwanza tunaanza na kwendana na sera Tanzania na ili tuweze kufikia uchumi wa kati nilazima kwanza tuhakikishe tuna Umeme wa uhakika wakutosha na usio katika katika Mara Kwa Mara tukishakuwa nao tutaweza kupata au kuwavutia wawekezaji wengi kuja kujenga viwanda hapanchini kwetu"alisema Mgaya 

alisema kuwa kama wazungu wameweza kumaliza tatizo la kukatika umeme katika nchi zao na kwa afrika alisema pia nchi ya Misri imeweza kumaliza tatizo hilo wanaamini na nchi yetu ya Tanzania wakisimama imara wanaweza kabisa tatizo hilo ,

alisema kuwa kitu kinachosababisha matatizo ya kukatika umeme kwanza ni miti kuwa karibu na miundo mbinu ya umeme kwa iyo watasafisha njia zote za umeme ,pia watabadilisha nguzo zote ambazo zimeoza na kuweka mpya na kubadilisha viungio au vifaa vyovyote vyakuunganisha umeme ambavyo vimechoka na wanaamini kwa kufanya hivyo tatizo hili la kukatika umeme mara kwa mara litakuwa limeisha kabisa. 
 Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la umeme (Tanesco ) Muhandisi Raimondi seya akimpatia cheti cha kushiriki semina mmoja wa wafanyakazi wa Tanesco anaetokea mkoani mwanza





No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad