HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, September 27, 2019

MAKAMU WA RAIS AHUTUBIA TAMASHA LA PILI LA UTALII ZANZIBAR

Sekta ya Nchini Utalii imetakiwa kushirikiana kwa pamoja na Wawekezaji na pamoja na watoa huduma ya Utalii Nchini kuweka nguvu zaidi kwenye kutoa matangazo ili kurahisisha Usafiri na kuweza kuleta Watalii kwa wingi Nchini.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema hayo Jana Usiku katika Tamasha la Maonesho ya pili ya Utalii Zanzibar yaliyofanyika katika Ukumbi wa Park Hyatt Shangani Zanzibar.

Mhe. Samia amesema ni vizuri kushirikiana na kuongeza nguvu, Jitihada katika kufanya kazi ili kukuza suala zima la Biashara ya Utalii Nchini ambapo pia amewataka Vijana kujitokeza kwa wingi kwenda katika maonesho hayo kuona kinachofanyika na kuweza kujifunza.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza kwenye hafla ya Tamasha la pili ya Utalii Zanzibar lililofanyika Jana usiku Park Hyatt Zanzibar.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikabidhi cheti kwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari Zanzibar Bibi Hadija Bakari kwa niaba ya Wizara yake kwa kufanikisha kufanikisha Tamasha la pili ya Utalii Zanzibar lililofanyika Jana usiku Park Hyatt Zanzibar.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikabidhi cheti kwa Katibu Mtendaji wa kamisheni ya Utalii Zanzibar Abdallah Mohamed kwa kuweza kufanikisha Tamasha la pili ya Utalii Zanzibar lililofanyika Jana usiku Park Hyatt Zanzibar.




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad