HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, September 12, 2019

KERO YA MAJI YAENDA KUWA HISTORIA MJI WA KISARAWE NA VITONGOJI VYAKE

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

Kukamilika kwa mradi wa Kisarawe kutanufausha mji mzima wa kisarawe, eneo la sekta viwanda na vitongoji jirani na mji huo.

Tatizo la Maji kwa Wananchi wa Kisarawe litabaki historia baada ya mradi wa ujenzi wa Tanki la maji lenye ujazo wa lita Milion sita kukamilika.

Mradi huo uliozinduliwa na Makamu wa Rais Mama Samia Hassan Suluhu utawanufaisha wananchu wa eneo la Kisarawe na maeneo ya Viwanda.

Ujenzi wa Mradi huo unasimamiwa na Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) ambao umechukua takribani miezi 12 kukamilika.

Akitoa taarifa ya kukamilika kwa mradi huo ambao kwa sasa mkandarasi anaendelea na kazi ya uunganishaji wa bomba, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Jamii DAWASA, Neli Msuya amesema kwa sasa Mkandarasi sambamba na mafundi kutoka Mamlaka hiyo wanaendelea na maunganisho ya bomba la nchi 16 kutoka Mtambo wa Ruvu juu kuelekea kwenye tanki la Kisarawe.

Amesema, maunganisho ya bom a hilo yanafanyika kwenye mradi wa Kibamba ambapo mafundi wapo katika hatua za mwisho kukamilisha.

Wakazi wa Kisarawe watanufaika na mradi huo ambapo wamekuwa na kero ya maji kwa muda mrefu na kukamilika kwake kutatatua changamoto hiyo pamoja na kuvutia wawekezaji kwenda kuwekeza kwenye maeneo ya viwanda.

Mradi wa Kisarawe unajengwa kwa fedha za ndani za Mamlaka ya Majisafi na Majitaka DAWASA na unagharimu takribani Bilioni 10 za kitanzania.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad