Meneja Kiongozi Mahusiano na Elimu kwa Umma wa NSSF, Lulu Mengele
akisisitiza jambo kwa wafanyakazi wa kampuni ya KK Security wakati wa zoezi la
kuwasajili.
SHIRIKA la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) limeendelea kuandikisha wanachama
wapya kutoka kwenye sekta binafsi na sekta isiyokuwa rasmi kupitia kampeni ya
NSSF na Marafiki iliyoanzishwa mwishoni mwa wiki iliyopita.
Kupitia kampeni hiyo NSSF imeweza kuandikisha wanachama wapya 472 kutoka
katika kampuni ya KK Security. Kampuni ya ulinzi ya KK security ilishukuru NSSF
kwa kuwapatia elimu ya hifadhi ya jamii kupitia kampeni ya NSSF na Marafiki
iliyofanikisha kusajili wafanyakazi 472 na NSSF.
Kampeni ya NSSF na Marafiki itazunguka Tanzania nzima kwa lengo la kuandikisha
wanachama wapya kutoka katika sekta binafsi na sekta isiyokuwa rasmi na
kuhakikisha waajiri wanawasilisha michango ya wafanyakazi wao kwa wakati.
Kufuatia mabadiliko ya sheria ya hifadhi ya Jamii ya mwaka 2018 NSSF inatoa
huduma ya Hifadhi ya Jamii kwa Sekta binafsi na Sekta Isiyokuwa Rasmi. Hivyo,
Kampeni hii itasaidia kuongeza wanachama kutoka katika sekta hizo.
Meneja Kiongozi wa Uendeshaji wa NSSF, Cosmas Sasi (kulia) akimuelekeza jinsi
ya kujaza fomu mfanyakazi wa Kampuni ya ulinzi ya KK Security wakati wa zoezi la
kuandikisha wanachama wapya 472 wa kampuni ya KK Security jijini Dar es
Salaam. Kushoto ni Meneja wa NSSF mkoa wa Kinondoni Hiza Kiluwasha wakati
akijaza taarifa za mwanachama mpya wa NSSF katika mifumo ya kielektroniki ya
Shirika.
Meneja Kiongozi wa Uendeshaji wa NSSF, Cosmas Sasi (kulia) akifuatilia
maelekezo anayopewa mwanachama mpya wa NSSF ambaye ni mfanyakazi wa
Kampuni ya ulinzi ya KK Security wakati wa zoezi la kuandikisha wanachama wapya
kampuni ya KK Security jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment