HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, July 30, 2019

MAKAMU WA RAIS AONYA MATUSI NA VITENDO VYA UDAHALILISHAJI MASOKONI



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimkabidhi Funguo ya Pikipiki Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith S. Mahenge Baada ya kuzindua rasmi Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko kwa ajili ya kuongeza Chachu ya kurahisisha Usafiri katika kufanikisha zoezi hilo, Jumla ya Pikipiki 14 zilitolewa kwa Mkoa wa Dodoma . Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiangalia Bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na Wajasiriamali Wanawake katika Mkoa wa Dodoma alipotembelea Mabanda ya Maonesho kwenye Uzinduzi wa Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akionesha Bango Juu kama ishara ya Uzindua rasmi Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko pamoja na ugawaji wa Pikipiki 14 kwa Maafisa wa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya wilaya ya Chamwino Dodoma kwa ajili ya kuongeza kurahisisha Usafiri katika kufanikisha kutokomeza Ukatili na Unyanyasaji kwa Wanawake na watoto . Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. Katikati Mwenyekiti wa ALAT Taifa na Meya wa Manispa ya Shinyanga Mhe. Gulamhafeez Z. Mukadam na Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu.
Baadhi ya Wafanyabiashara wa Masokoni Wanawake na Wanancho wa Dodoma, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, alipokuwa akihutubia kwenye Hafla ya Uzinduzi wa Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Mratibu wa Umoja wa Mataifa Tanzania Alvaro Rodriquez walipokutana kwenye Hafla ya Uzinduzi wa Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshuhulikia Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji wanawake (UN WOMEN) Bibi. Hadon Addou walipokutana kwenye Hafla ya Uzinduzi wa Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 
Mwenyekiti wa ALAT Mhe Gulamhafeez Mukadam,akizungumza na Wafanyabishara Wanawake wa Masokoni na Wananchi wa Dodoma kwenye Hafla ya Uzinduzi wa Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akihutubia Wafanyabishara Wanawake wa Masokoni na Wananchi wa Dodoma kwenye Hafla ya Uzinduzi wa Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 

Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akizungumza na Wafanyabishara Wanawake wa Masokoni na Wananchi wa Dodoma kwenye Hafla ya Uzinduzi wa Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akikata Utepe kuzindua rasmi Mradi wa kutokomeza vitendo vya Unyanyasaji na Udhalilishaji Dhidi ya Wanawake na Watoto katika maeneo ya Masoko pamoja na ugawaji wa Pikipiki 14 kwa Maafisa wa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya wilaya ya Chamwino Dodoma kwa ajili ya kuongeza kurahisisha Usafiri katika kufanikisha kutokomeza Ukatili na Unyanyasaji kwa Wanawake na watoto . Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30,2019 katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 
Makamu wa Rais wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema watu wanatumia matusi ni watu waliokosa malezi kwa namna tofauti tangu wakiwa wadogo hivyo kuitaka Jamii ya Watanzania kutumia nguvu nyingi katika malezi ya watoto ili kuepukana na athari za ukosefu wa malezi ukubwani. 

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema hayo leo jijini Dodoma katika hotuba yake ya uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza vitendo vya unyanyasaji na udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto katika maeneo ya masoko na zoezi la ugawaji wa pikipiki kwa waataalam wa maendeleo ya Jamii leo Jijini Dodoma. 

Aidha Makamu wa Rais amekemea wanaume wanaotumia lugha ya matumisi katika maeneo ya masoko kuwa yanasabababisha wakina mama wafanya biashara Sokoni kukosa uhuru na hata kushindwa kuleta watoto wao sokoni kwa ajili ya kuwasaidia kwa kutopenda vijana wao kusikia lugha isiyokuwa na maadili. 

“Mnawazalilisha wanawake kwa kuwatukana matusi kwa kutumia viungo vyao, kuwashika au kuwapapasa bila idhini yao kwanini nyie wanaume msishikane wenyewe vitendo vya kuwazalilisha wanawake havikubaliki kabisa’’. Alisisitiza Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan. 

Katika hotuba yake hiyo Makamu wa Rais wa Tanzania amesema vitendo hivyo vya ukatili havikubaliki na ndio maana ya ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ibala ya 168 c inasema wanawake wanayo haki ya kulindwa dhidi ya unyanyasaji wa aina yoyote ile hivyo hatua za kukomesha vitendo vya ukatili dhidi yao ni utekelezaji wa ilani hiyo. 

Pamoja na kukemea vitendo hivyo Makamu wa Rais wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewataka wanaume wanaonyanyaswa Kijinsia wasione aibu bali watoe taarifa kwenye dawati la Jinsia la Jeshi la Polisi ili Serikali iweze kupata takwimu sahihi ili iweze kufanyia kazi chanagamoto hiyo. 

Aidha Makamu wa Rais amehoji wanawake walio katika Kamati ya Soko kwanini wanafumbia macho vitendo vya ukatili ili hali wao ni viongozi watoa maamuzi sokoni hapo na kuonya kuwa uenda na wao wanachangia kuendelea kuwepo kwa ukatili katika maeneo ya sokoni. 

Makamu wa Rais amewataka viongozi wa masoko nchini kuhakikisha wanafanyia kazi tabia ya watoto wadogo kufanya biashara sokoni kwa lengo la kusaidia familia na kuutaka uongozi wa soko kuwahoji na kuwarudisha shuleni ili kusaidia kukata mnyororo wa umasikini wa familia kwani mtoto akipata elimu inamsaidia kutumia elimu yake kupambana na umasikini. 

Kwa upande wake Waziri wa Afya, MAendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amemwomba Makamu wa Rais kuagiza Halmashauri zote nchini kuacha kutoa kiwango kidogo cha mikopo kwa akina na mama na waongeze kiwango cha fedha ili wakinamama wapate miradi ya maana ya biashara kupitia makato ya 4% ya mapato ya kwa Halmashauri. 

“Unakuta kikundi cha akina mama watano wapewa mkopo wa laki tano nakugawana fedha kidogo hii ni pesa gani ndio maana wakina mama wanaishia kuila na kushindwa kufanya marejesho kwa kuwa fedha hii inakuwa haitoshi kufanya chochote’’ Aliongeza Waziri Mwalimu. 

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu amesema Wizara kwa kushirikiana na wadau wataendelea kutafuta na kugawa Pikipiki kwa Mikoa mingine baada ya Mkoa wa Dodoma ili kuwawezesha Maafisa Maendeleo nchini kutoa elimu kwa jamii kuhusu vitendo vya ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto. 

Dkt. Jingu amesema kuwa Wizara imetoa pikipiki 25 kwa mkoa wa Dodoma na mapema mwezi ujao itatoa pikipiki kumi na tano kama hizo kwa Mkoa wa Rukwa ili kuwawezesha Maafisa Maendeleo Mkoani humo kutumia usafiri huo kuelimisha wananchi kuhusu ukatili na unyanyasaji dhidi ya Wanawake na Watoto. 

Naye Beatrice Siame ambaye ni Mwakilishi wanawake Soko la Majengo ameiomba Serikali kusimamia usawa wa kijinsia katika maeneo ya kazi ili wanawake waweze kunufaika na kuwezeshwa kiuchumi lakini pia akibainisha kuwa changamoto ya soko ya bidhaa zao ni kikwazo katika kumwendeleza mwanamke kiuchumi. 

Uzinduzi wa Mradi wa kupinga unyanyasaji na udhalilishaji wanawake kijinsia katika Masoko ni hatua muhimu ya utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Kutomeza Vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto unaolenga kutokomeza vitendo vya ukatili Nchini kwa 50% ifikapo 2022.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad