HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, April 3, 2019

YALIYOJIRI LEO BUNGENI JIJINI DODOMA

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza  jambo wakati akiongoza Kikao cha 2 cha Mkutano wa 15 wa Bunge la 11 leo Bungeni Jijini Dodoma.
Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (kulia mbele) akiteta jambo na Spika wa Bunge la Misri, Mhe. Dkt. Ali Abdel Aal Sayyed Ahmed (katikati mbele) katika jukwaa la Wageni wa Spika Bungeni Jijini Dodoma, Mhe. Dkt. Ali kalitembelea Bunge katika ziara ya kuboresha mahusiano baina ya nchi hizi mbili. Kushoto mbele ni Rais wa Seneti ya Burundi, Mhe. Reverin Ndikuriyo
Mhamasishaji Maarufu wa Timu ya Taifa Stars, Ndg. Peter Mollel alimaarufu kama Pierre Liquid akitambulishwa leo Bungeni Jijini Dodoma na Spika wa Bunge, Mhe. Job ndugai (hayupo kwenye picha) aliemualika kama mgeni wake.
Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (mbele) akielezea ukaaji ndani ya Bunge kwa Spika wa Bunge la Misri, Mhe. Dkt. Ali Abdel Aal Sayyed Ahmed (kulia) na Rais wa Seneti ya Burundi, Mhe. Reverin Ndikuriyo (wa pili kulia) pale ugeni kutoka nchi hizo ulipotembelea leo Bungeni Jijini Dodoma. Katika ziara ya kuboresha mahusiano baina ya nchi hizo mbili na Tanzania. Wageni wengine ni maofisa kutoka Bunge la Misri, Burundi na Tanzania
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Spika wa Bunge la Misri, Mhe. Dkt. Ali Abdel Aal Sayyed Ahmed alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma, Katika ziara ya kuboresha mahusiano baina ya nchi hizi mbili. Katikati ni Mkalimani Ndg. Alaa Salah Abdelwahed.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akizungumza na Spika wa Bunge la Misri, Mhe. Dkt. Ali Abdel Aal Sayyed Ahmed alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma. Katika ziara ya kuboresha mahusiano baina ya nchi hizi mbili   
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kushoto) akizungumza na ugeni kutoka Bunge la Misri ulioongozwa na Spika wa Bunge la Misri, Mhe. Dkt. Ali Abdel Aal Sayyed Ahmed (watatu kushoto) walipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma, Katika ziara ya kuboresha mahusiano baina ya nchi hizi mbili. Kushoto ni Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akimpatia zawadi ya picha yenye Jengo la Bunge Spika wa Bunge la Misri, Mhe. Dkt. Ali Abdel Aal Sayyed Ahmed alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma, Katika ziara ya kuboresha mahusiano baina ya nchi hizi mbili. Kulia ni Mkalimani Ndg. Alaa Salah Abdelwahed
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kulia) akiongozana na Spika wa Bunge la Misri, Mhe. Dkt. Ali Abdel Aal Sayyed Ahmed (katikati) alieambatana na ugeni kutoka Bunge la Misri wakielekea katika Ukumbi wa Pius msekwa Kuhutubia Bunge tukio lililofanyika leo Bungeni Jijini Dodoma, Wageni walikuja katika ziara ya kuboresha mahusiano baina ya nchi hizi mbili. 


Mawaziri, Manaibu Waziri, Wabunge na Wafanyakazi wa Ofisi ya Bunge wakiwa katika Ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Jijini Dodoma, wakifuatilia hotuba ya Spika Ndugai pale ugeni kutoka Bunge la Misri, Burundi na Cameroon ulipotembelea Bunge la Tanzania, Kwa ziara ya kuboresha mahusiano baina ya nchi hizo na Tanzania.

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na ugeni kutoka Bunge la Misri, Burundi na Cameroon pamoja na Mawaziri, Manaibu Waziri, Wabunge na Wafanyakazi wa Ofisi ya Bunge katika Ukumbi wa Pius Msekwa leo Bungeni Jijini Dodoma. Ugeni huo ulitembelea Bunge kwa ziara ya kuboresha mahusiano baina ya nchi hizo na Tanzania. (PICHA NA DEONISIUS SIMBA - OFISI YA BUNGE)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad