HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, April 29, 2019

WAZIRI WA ELIMU AFANYA UKAGUZI WA HATUA ZA MAANDALIZI YA UWEKAJI JIWE LA MSINGI JENGO LA CHUO KIKUU MZUMBE KAMPASI YA MBEYA

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhe. Prof. Joyce Ndalichako leo ametembelea na kukagua hatua za maandalizi ya ujenzi wa Jengo la Taaluma na Utawala la Chuo Kikuu Mzumbe Kampasi ya Mbeya, ambapo amepongeza Uongozi wa Chuo Kikuu Mzumbe kwa hatua za ujenzi ulipofikia.

Akiwa ameambatana na Kaimu Mkuu wa Chuo hicho Pro. Lughano Kusiluka, Prof Ndalichako amemwelekeza Mkandarasi wa Ujenzi kuhakikisha kufikia Juni 2019 ujenzi wa Jengo hilo kuwa umekamilika kama ilivyopangwa.

Kukamilika kwa ujenzi kutawezesha jumla ya wanafunzi 900 kupata vyumba vya madarasa mbali na kumbi za mikutano na ofisi za uendeshaji. Jengo hilo linatarajiwa kuwekwa jiwe la Msingi na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Joseph Magufuli Mei 1, 2019.
 
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Prof. Joyce Ndalichako akiongozwa na Mkandarasi wa mradi akikagua vyuma vya madarasa mara alipowasili kukagua ujenzi wa jengo la ghorofa tano la Taaluma na Utawala linalotazamiwa kumalizika mwezi Juni,2019. Pamoja naye ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Prof. Lughano Kusiluka, Naibu Mawakamu Mkuu wa Chuo Utawala na fedha Prof. Ernest Kihanga na wasimamizi wa ujenziWaziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce Ndalichako akiweka saini kwenye kitabu cha wageni kwenye eneo la ujenzi wa Jengo la Taaluma na Utawala la chuo Kikuu Mzumbe Kampasi ya mbeya mara tu baada ya kuwasili. Aliyeshika kitabu ni Injiani Thadeus Koyanga na kushoto anayeshuhudia tukio hilo ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Profesa Lughano Kusiluka ( Mwenye Kaunda suti kushoto) Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce Ndalichako (kushoto) akiwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Profesa Lughano Kusiluka ( Mwenye Kaunda suti kushoto) pamoja na Mkandararasi na wajenzi; wakikagua ramani ya jengo la Taaluma na Utawala la Chuo Kikuu Mzumbe Kampasi ya Mbeya. Profesa Ndalichako (katIkati) akikagua mahali litakapojengwa jiwe la msingi ambalo litawekwa rasmi na Mhe. Rais wa Jamhuri wa Muuungano wa Tanzania Dr.John Pombe Joseph Magufuli Mei 1, 2019. Kushoto ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Profesa Lughano Kusiluka na kulia ni Mkadarasi wa Ujenzi Injinia Thedeus Koyanga (mwenye shati la mikono mirefu) akifuatiwa na Profesa Ernest Kihanga Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Utawala na Fedha.Mhe. Profesa Joyce Ndalichako alikagua muonekano wa nje wa jengo la Taaluma na Utawala la chuo Kikuu Mzumbe Kampasi ya Mbeya pamoja na kukagua usafi wa mazingira, alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi kabla Mhe. Rais Dkt John Pombe Magufuli hajafika kuweka jiwe la msingi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad