HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, April 29, 2019

KAMBI ZA KITAALUMA SIMIYU ZITAKUWA ENDELEVU - RC MTAKA

Mkuu wa Mkoa.wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na wanafunzi wa Kidato Cha Sita Mkoani humo, wakati wa kufunga Kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi hao, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019
Baadhi ya wanafunzi wa Kidato Cha Sita Mkoani Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa kufunga Kambi ya Kitaaluma ya Wanafunzi hao, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo.
Aliyekuwa mlezi(Patron) wa kambi ya kitaaluma ya kidato cha sita kwa wanafunzi wa kidato cha Sita mkoani Simiyu, Mwl.Pimbili Chalya kutoka Mwandoya, akitoa tathmini ya kambi hiyo , iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka.
Joseph Mathias Mwanafunzi kutoka Shule ya Sekondari Bariadi akitoa tathmini ya kambi ya kitaaluma ya kidato cha sita mkoani Simiyu, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka.
Mwanafunzi wa kidato cha Sita Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, akitoa burudani ya wimbo, wakati wa kufunga Kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi hao, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka.
Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato kutoka Mkoani Mwanza, Nicodemo Ntabindi akizungumza na wanafunzi wa Kidato Cha Sita Mkoani Simiyu, wakati wa kufunga Kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi hao, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka.
Mwalimu Dennis Wasagara ambaye pia ni mzazi akizungumza na wanafunzi wa Kidato Cha Sita Mkoani Simiyu, wakati wa kufunga Kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi hao, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka.
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Mwl. Kuyunga Jackson akitoa tathmini ya kambi ya kitaaluma ya kidato cha sita mkoani Simiyu, wakati wa kufunga kambi hiyo , iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka.

Na Stella Kalinga, Simiyu

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema Kambi za Kitaaluma mkoani Simiyu kwa wanafunzi wa darasa la saba, kidato cha nne na kidato cha Sita, ambayo ni madarasa yanayofanya Mitihani ya Taifa ya kuhitimu elimu ya Msingi na Sekondari zitakuwa endelevu.

Mtaka amesema hayo Aprili 28, 2019 wakati akihitimisha Kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha sita iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, ikihusisha wanafunzi 1166 kutoka katika shule 12 mkoani hapa.

Amesema Mkoa utaendelea kufanya jitihada na kuboresha zaidi kambi hizo huku akieleza kuwa ameshawaelekeza Wakurugenzi wa Halmashauri zote mkoani humo kutenga fedha kwa ajili ya motisha kwa walimu na wanafunzi watakaokuwa wakifanya vizuri.

“Kambi za kitaaluma  zitaendelea kuwepo katika kipindi chote nitakacho kuwepo na tutaendelea kuboresha; mwaka huu nimewaambia Wakurugenzi ni lazima kila Halmashauri itenge fedha kwa ajili ya motisha katika elimu, motisha kwa walimu na wanafunzi wanaofanya vizuri” alisema Mtaka.

Katika hatua nyingine Mtaka amewashukuru walimu, wanafunzi na wadau mbalimbali waliochangia kufanikisha kambi ya kidato cha sita, huku akiwasisitiza wanafunzi wa hao kuendeleza juhudi walizozionesha wakiwa kambini na kutumia mbinu walizopewa na walimu mahiri ili waweze kufanya vizuri mitihani yao ya mwisho.

Naye Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato kutoka Jijini Mwanza, Nicodemo Ntabindi amewaonya wanafunzi wa Kidato cha sita kutojihusisha na masuala ya mapenzi badala yake wajikite katika masomo tu kwa sasa ili waweze kufikia ndoto zao.

Kwa upande wao wanafunzi waliokuwepo katika kambi hiyo ya Kitaaluma wamesema kambi hiyo imekuwa msaada kwa wanafunzi kwa kuwa imechangia kuwasaidia kupata ufumbuzi wa mada ngumu zilizokuwa zinawapa shida na kuahidi kufanya vizuri katika mtihani wa Taifa kutokana na namna walivyoandaliwa vema.

“Tunashukuru uwepo wa kambi hii maana imetusaidia kupata maarifa ya namna ya kujibu maswali kwenye mitihani, lakini tumeweza kusaidiwa na walimu kutatua mada ngumu ambazo zilikuwa zinatushinda, ninaamini kwa namna tulivyoandaliwa hatutamuangusha Mkuu wetu wa Mkoa” alisema mwanafunzi Farida Omary.

“Kambi hizi hazijafanyika popote hapa nchini tunamshukuru sana Mkuu wa Mkoa kwa kuja na wazo la kuwa na kambi kwa sababu tumejifunza mengi, tumekutana na wenzetu wa shule mbalimbali hapa mkoani kwetu na tukapata maarifa ambayo awali hatukuwa nayo, tuna imani tufanya vizuri “ alisema mwanafunzi Casto Nyakarungu.

Katika kambi hii Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu, imetoa shilingi milioni 12 kwa ajili ya motisha kwa walimu waliokuwa wakifundisha kambini hapo na imeahidi kutoa shilingi milioni nne kwa mwanafunzi atakayepata ‘division one, pointi tatu’ na kuwa miongoni mwa wanafunzi kumi bora Kitaifa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad