Na Ahmed Mahmoud Arusha
Chama cha wananchi. CUF kinajipanga kuhakikisha kinashiriki kikamilifu
katika Chaguzi mbali mbali hapa nchini ikiwemo Chaguzi za serikali za
mitaa na uchaguzi mkuu 2020 Kwa kuimarisha chama maeneo mbali mbali
nchini.
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Taifa ulinzi wa chama hicho Masoud
wakati alipofanya mahojiano na waandishi wa habari jijini Arusha baada
ya kutembelea mikoa ya Dodoma Manyara na Arusha kwenye ziara yake ya
kuimarisha chama hicho kwenye mikoa mbali mbali nchini.
Amesema kuwa chama cha wananchi CUF kinajipanga Sawa kuweza kutoa
ushindani katika Chaguzi hizo baada ya kutoka katika mgogoro wa
viongozi waliondoka na kukimbilia ACT hivyo kimeweka mikakati ya
kuimarisha chama hicho kujianda na Chaguzi
"Tumejipanga kukiimarisha chama kushiriki Chaguzi Kwa mafanikio ndio
maana tumapita kote kuona chama kinahakikisha kinashinda kwenye
Chaguzi zilizo mbele yetu"
Amesema kuwa msingi mkubwa wa chama hicho ni UMOJA Kati ya wanachama
na kuimarisha misingi ya chama Kwa kuweza kupata viongozi Bora
watakaosaidia jamii kutoka kwenye Lindi la umaskini kuelekea kwa
kutekeleza Sera ya utajirisho Kwa watanzania.
Awali akimkaribisha mkurugenzi huyo Mwenyekiti wa chama hicho Wilaya
ya Arusha Omary Selusingo aliwataka viongozi wa chama hicho kuwa kitu
kimoja kujenga.chama Kwa misingi ya umoja na mshikamano ili kuweza
kufikia lengo.
Amesema kuwa mikakati ya chama hicho ni kuona changamoto mbali mbali
zikitatuliwa ikiwemo chama mkoani hapa kuwa na ofisi zake kila wilaya
sanjari na vitendeakazi vitakavyosaidia kukiimarisha chama mkoani
hapa.
"Chama mkoani hapa kinakabiliwa na changamoto ya kutokuwa na ofisi ila
tumeweka mikakati ya kuhakikisha kata tano ndani ya Jiji la Arusha
chama kinashinda Kwa kuanzia na Chaguzi za serikali za mitaa"
No comments:
Post a Comment