HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, March 14, 2019

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU NA KAMATI YA PAC YAKAGUA MIRADI YA UJENZI

 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Moshi Selemani Kakoso, akisisitiza jambo kwa  Naibu Mawaziri wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Elias Kwandikwa na Atashasta Nditiye, wakati kamati hiyo ilipokagua ukarabati wa Kiwanja cha Ndege cha Dodoma.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa akifafanua jambo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, wakati kamati hiyo ilipokagua ukarabati wa Kiwanja cha Ndege cha Dodoma. Wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Moshi Selemani Kakoso.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi na Mawasiliano), Atashasta Nditiye, akifafanua jambo kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Moshi Selemani Kakoso, wakati kamati hiyo ilipokagua ukarabati wa Kiwanja cha Ndege cha Dodoma. 
 Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Dodoma,  Bertha Bankwa, akielezea mkakati wa uboreshaji wa kiwanja hicho kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, wakati kamati hiyo ilipokikagua.
 Muonekano wa barabara ya kuruka na kutua ndege katika Kiwanja cha Ndege cha Dodoma. Barabara hiyo imerefushwa kutoka mita 2,000 hadi mita 2,500.
 Mhandisi Kedrick Chawe kutoka Wakala wa Barabara (TANROADS), akionesha ramani ya Kiwanja cha Ndege cha Msalato kitakavyokuwa mara baada ya awamu ya kwanza ya ujenzi wake kukamilika kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, wakati kamati hiyo ilipokagua eneo ambalo kiwanja hicho kitajengwa.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Arch. Elius Mwakalinga, akisoma taarifa ya mradi wa barabara ya Iringa-Dodoma (Km 260) kwa wajumbe wa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), katika Ofisi za Bunge jijini Dodoma, leo.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Naghenjwa Kaboyoka, akikagua ubora wa lami katika eneo la Nkulabi, barabara ya Iringa-Dodoma (Km 260), wakati kamati hiyo ilipokagua barabara hiyo leo.
 Mkurugenzi Msaidizi wa Barabara kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhandisi John Ngowi, akifafanua jambo kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), walipokagua barabara ya Iringa-Dodoma (Km 260).
Muonekano wa Barabara ya Iringa -Dodoma (Km 260) sehemu ya Migori- Fufu (Km 93.80) ambayo ujenzi wake umekamilika kwa kiwango cha lami.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad