HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, February 5, 2019

YALIYOJIRI LEO BUNGENI JIJINI DODOMA

  Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Job Ndugai akizungumza mara baada ya Bunge kurejea Jijini Dodoma. Spika ametoa Taarifa fupi kuhusu Kingora cha hatari kilicholia kuashiria hali ya hatari  Bungeni  kuwa hakukuwa na hatari yeyote.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania Mhe.Dkt Tulia Ackson akiuliza swali leo Bungeni Jijini Dodoma.

  Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira Mhe.Musa Sima akijibu maswali mbalimbali ya wabunge Bungeni leo Jijini Dodoma.
 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof . Palamagamba Kabudi akijibu hoja mbalimbali za wabunge leo Bungeni Jijini Dodoma.
Katibu wa Bunge Mhe.Stephen Kagaigai akiteta jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Vijana, Ajira  na Wenye Ulemavu Mhe,Jenista Mhagama,Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe.William Lukuvi na Mbunge wa Arusha Mjini Mhe.Godbless Lema wakati Bunge lilipositishwa kwa muda baada ya King’ora cha kuahsiria hatari  kulia leo Bungeni JIjini  Dodoma.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama,Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Uwekezaji Mhe.Angellah Kairuki wakijadili jambo na Mbunge wa Ubungo Mhe.Said Kubenea na Mbunge wa Kigoma kaskazini Mhe.Zitto Kabwe leo Bungeni Jijini Dodoma.
 Wageni mbalimbali wakifuatilia shughuli mbalimbali za Bunge leo Jijini Dodoma.

 Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa  akifurahia jambo na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Wenye Ulemavu Mheshimiwa Stella Ikupa nje ya Ukumbi wa Bunge.Dodoma leo Februari 5/2019
 Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa  akisalimiana na baadhi ya Wabunge na Wananchi mbalimbali katika Viwanja vya Bunge, Jijini Dodoma. leo Februari 5/2019
Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa  akiwa katika maongezi na , Kaimu Askofu Mkuu wa Kanisa la Assemblies of God Tanzania(TAG). Dkt. Magnus Mhiche wakati alipomtembelea Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma. Februari 5/2019

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad