HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, February 26, 2019

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA DAKTARI BINGWA WA UPASUAJI WA UBONGO NA MISHIPA YA FAHAMU

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu Profesa Zhao Yuanil kutoka Hospitali ya Kimataifa ya Chuo Kikuu cha Peking cha Beijing nchini China mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika Mazungumzo na Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu Profesa Zhao Yuanil kutoka Hospitali ya Kimataifa ya Chuo Kikuu cha Peking cha Beijing nchini China aliyeambatana na ujumbe wake pamoja na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Profesa Lawrence Maseru na Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Respicious Boniface Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu Profesa Zhao Yuanil kutoka Hospitali ya Kimataifa ya Chuo Kikuu cha Peking cha Beijing nchini China wanne kutoka kulia, Balozi wa China hapa nchini Wang Ke watatu kutoka kulia pamoja Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Respicious Boniface. Wengine katika picha ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, Balozi Zuhura Bundala pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Profesa Lawrence Maseru.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu Profesa Zhao Yuanil kutoka Hospitali ya Kimataifa ya Chuo Kikuu cha Peking cha Beijing China wanne kutoka kulia mara baada ya kumaliza kupiga picha ya kumbukumbu Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi zawadi ya Kinyago Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo  na Mishipa ya Fahamu Profesa Zhao Yuanil kutoka Hospitali ya Kimataifa ya Chuo Kikuu cha Peking cha Beijing China mara baada ya mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kulia ni Balozi wa China hapa nchini Wang Ke akishuhudia.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Balozi wa China hapa nchini Wang Ke mara baada ya kumaliza mazungumzo na Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo  na Mishipa ya Fahamu Profesa Zhao Yuanil kutoka Hospitali ya Kimataifa ya Chuo Kikuu cha Peking cha Beijing China. PICHA NA IKULU

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad