HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, February 27, 2019

MAKAMU WA RAIS AFANYA ZIARA WILAYANI SHINYANGA

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kutoka kwa Mhandisi Edward K. Mulumba (kulia) wa Wizara ya Maji  yanayohusu maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ofisi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji taka Shinyanga (KASHWASA). (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Picha ya Jengo la Madarasa ya Chuo cha Ualimu SHYCOM ambalo Makamu wa Rais alitembelea na kutaka kujua kwa nini ujenzi wake umesimama. Makamu wa Rais yupo mkoani Shinyanga katika ziara ya kukagua na kuhamasisha shughuli za maendeleo. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa haamini macho yake kuona uchafu uliokithiri mara baada ya kutembelea jiko la kupikia chakula cha wanafunzi wa Chuo Cha Ualimu SHYCOM wengine pichani ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Taleck (kushoto) na Mkuu wa Chuo hicho John Nandi. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Mwanafunzi wa Chuo Cha Ualimu SHYCOM Happyness Kasuku akimueleza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) changamoto ya maktaba ya kusomea ambayo ni ndogo na ina vitabu vichache. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akkizungumza na wanafunzi wa Chuo cha Ualimu SHYCOM mkoani Shinyanga mara baada ya kutembelea chuo hicho na kukagua ukarabati na ujenzi wa miundombinu. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Wanafunzi Nchambi Nsile (kulia) anayesoma darasa la 7 akiwa amempakata mwenzake Nyazobe Sembe darasa la 4 wa Shule ya Msingi Jumuishi Buhangija wakati wa kumsikiliza Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye alitembelea shule hiyo na kufungua Bwalo.
Makamu wa Rais yupo ziara ya kikazi mkoani Shinyanga. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Shinyanga (CCM) Mhe. Azza Hilal Hamad akiwa amempakata mmoja wa wanafunzi Shule ya Msingi Jumuishi Buhangija wakati wakimsikiliza Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) ambaye alitembelea shule hiyo na kufungua Bwalo. 
Makamu wa Rais yupo ziara ya kikazi mkoani Shinyanga. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wanafunzi wa shule ya Msingi Jumuishi Buhangija (hawapo pichani) mkoani Shinyanga. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo ya namna kutoka kwa Msanifu wa Pamba Bi. Sharifa Salum (kushoto) mara baada ya kutembelea maabara ya pamba katika Ofisi ya Bodi ya Pamba mkoani Shinyanga. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo ya namna kutoka kwa Msanifu wa Pamba Bw. Dotto Ntumba (kushoto) mara baada ya kutembelea maabara ya pamba katika Ofisi ya Bodi ya Pamba mkoani Shinyanga. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad