HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, January 25, 2019

WAZIRI BITEKO AMALIZA MGOGORO KATI YA KAMPUNI YA BEAL NA MTL


Waziri wa Madini, Doto Biteko amemaliza mgogoro uliokuwepo kati ya Kampuni ya Barrick Exploration Africa Limited (BEAL) na Megagems Tanzania Limited (MTL) uliodumu kwa muda mrefu. MTL ambaye ni mlalamikiji alikuwa anadai kulipwa kiasi cha Dola za Marekani 10,000 na Kampuni ya BEAL.

Akisuluhisha mgogoro huo Waziri Biteko ameitaka Kampuni ya BEAL kumlipa mlalamikaji kwa kuwa vibali vyote vinaonesha kuwa anastahili kulipwa. Kikao hicho kimefanyika leo tarehe 25 Januari, 2019 jijini Dodoma katika Ofisi ya Waziri wa Madini, Doto Biteko.
 Waziri wa Madini, Doto Biteko akishuhudia Mwakilishe wa Kampuni ya Barrick Exploration African Limited (BEAL), Janet Lekashingo akipeana mkono na mmiliki wa kampuni ya Megagems Tanzania Limited (MTL) baada ya kufikia mwafaka wa mgogoro wao wa MTL kulipwa haki yake.
 Kamishna wa Madini, Mhandisi David Mulabwa (wa kwanza kushoto) akifatilia  kikao cha kusuluhisha mgogoro kati ya Kampuni ya Barrick Exploration Africa Limited (BEAL) na Megagems Tanzania Limited (MTL). Wengine katika picha ni Mwanasheria wa Wizara, Godfrey Nyamsenda (wa pili kushoto), Mwanasheria wa Novelty Advocate Joseph Asenga na Mmiliki wa Kampuni ya MTL, Suleiman Nasib.
 Mwakilishi wa Kampuni ya Barrick Exploration African Limited (BEAL), Janet Lekashingo akimkabidhi Waziri wa Madini, Doto Biteko nyaraka kwa ajili ya kupitia kabla ya kumaliza Mgogoro uliokuwepo kati ya Kampuni ya Barrick Exploration Africa Limited (BEAL) na Megagems Tanzania Limited (MTL).
 Waziri wa Madini, Doto Biteko akipitia nyaraka iliyokabidhiwa kwake na Mwakilishe wa Kampuni ya Barrick Exploration African Limited (BEAL), Janet Lekashingo (hayupo pichani) kabla ya kumaliza mgogoro kati ya Kampuni ya Barrick Exploration Africa Limited (BEAL) na Megagems Tanzania Limited (MTL). 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad