HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, January 11, 2019

FAO Yaahidi Ushirikiano Zaidi na Serikali

Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) limeahidi kuendeleza ushirikiano na Serikali ya Tanzania katika kuiinua sekta ya kilimo nchini. Hayo yamesemwa na Ndugu muwakilishi wa Shirika hilo nchini Ndugu Fred Kafeero alipokutana na Naibu Waziri wa Kilimo, Innocent Bashungwa katika ofisi za FAO jijini Dar es Salaam.

Katika kikao hicho Ndugu Kafeero alieleza namna ambavyo shirika hilo limekuwa mstari wa mbele kushirikiana na serikali katika kutunga sera na kuandaa mikakati yenye lengo la kuhakikisha Tanzania inasonga mbele katika kilimo. Amesema FAO kwa miaka ya karibuni imefanya kazi kwa ukaribu na Shirika la Takwimu Tanzania (NBS) kwa kulijengea uwezo wa ndani unaoisaidia pia serikali katika ufuatiliaji wa bei ya mazao nchini.

Nae Naibu Waziri wa Kilimo Innocent Bashungwa alimueleza muwakilishi huyo mpango wa Serikali ya awamu ya tano wa kuorodhesha wakulima wote nchini ili kuweza kupanga vizuri kuhakikisha kila mkulima anapata huduma muhimu zitakazomsaidia toka hatua za uandaaji shamba mpaka masoko, na kuiomba FAO kama mdau muhimu wa kilimo kuipa Serikali ushirikiano ambapo Ndugu Kafeero aliahidi kulifanyia kazi ombi hilo.

Aidha, Naibu Waziri Bashungwa ameomba IFAD (shirika tanzu la FAO) isaidie Serikali kwa kushirikiana na  Benki ya Kilimo nchini kuwapatia wakulima nchini kupata mikopo ya riba nafuu, kusaidia taasisi za utafiti wa kilimo nchini, kujenga uwezo wa kuzalisha mbegu za mazao ya kimkakati na mchanganyiko, kujenga maghala ya kuhifadhi mazao ili kupunguza hasara wakati wa mavuno shambani (post harvest losses) na kuwajengea uwezo maafisa ugani nchini kufundisha kilimo cha tija kwa wakulima nchini. 

Mwakilishi wa FAO nchini amekubaliana na Naibu Waziri Bashungwa kufanyika kikao mwezi Februari 2019 cha Wizara ya Kilimo, FAO na mashirika mengine ya kimataifa yanayohusika na kilimo nchini kujadili vipaumbele tajwa ili kuijengea uwezo Wizara wa kuweza kuihudumia sekta ya kilimo nchini ili iendelee kukua na kutimiza azma ya Serikali ya awamu ya tano ya kufikia uchumi wa kati
 Naibu Waziri wa Kilimo Innocent Bashungwa akizunguza na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) Ndugu Fred Kafeero na msaidizi wa mwakilishi huyo Ndugu Charles Tulahi katika ofisi za shirika hilo jijini Dar es Salaam
 Mheshimiwa Innocent Bashungwa akimueleza muwakilishi wa FAO nchini mipango ya Serikali ya awamu ya tano katika kuinua kilimo
 Fred Kafeero akimkabidhi Naibu Waziri wa Kilimo baadhi ya machapisho yanayoonyesha mikakati ya FAO 
 Naibu Waziri wa Kilimo Innocent Bashungwa akiagana na msaidizi wa muwakilishi FAO nchini Ndugu Charles Tulahi mara baada ya kumalizika kwa kikao
 Innocent Bashungwa akimsikiliza kwa makini muwakilishi wa Shirika la FAO wakati akimuelezea shughuli za shirika hilo
Naibu Waziri wa Kilimo Innocent Bashungwa akiagana na msaidizi wa muwakilishi FAO nchini Ndugu Charles Tulahi mara baada ya kumalizika kwa kikao

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad