HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, January 10, 2019

BILIONEA WA DUNIA ABWAGANA NA MKEWE

Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
JEFF Bezos (54) ambaye anashikilia nafasi ya kwanza akiwa mtu mwenye utajiri zaidi duniani akimiliki utajiri wa dola za kimarekani zaidi ya Bilioni 136.2 akimzidi Bill gates kwa dola za kimarekani Bilioni 45 ametangaza kuachana na mkewe MacKenzie Benzos (48) waliyedumu kwa miaka 25 ya ndoa.

Kupitia ukurasa kwake wa Twitter Jeff ameandika kuwa "Baada ya muda mrefu katika mapenzi na kujaribu kuachana  tumeamua kutengana na tutaendelea kuishi kama marafiki" Ameandika Bezos.

Licha ya kutangaza uamuzi huo sababu za kutengana kwao hawajaziweka wazi na inasemekana kuwa talaka hiyo itakuwa ghali zaidi kuwahi kutokea.

Wawili hao walioana mwaka 1993 na kujaliwa watoto wanne huku  MacKenzie akiwa mwandishi huku wakiwa wamiliki wa Amazon.com, kampuni za anga za juu ya Blue Orgin na jarida la biashara la Bloomberg na Washington post.

Jeff alimpiku Gate na kuwa mtu tajiri zaidi duniani mwaka 2017 akiwa na utajiri wa dola za kimarekani bilioni 90.6 na inasemekana Jeff anaweza kuporomoka katika nafasi hiyo kama atatoa nusu ya umiliki wa mali zake kwa MacKenzie.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad