HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, December 11, 2018

Ukaguzi wa mabasi ni endelevu

Mkurugenzi wa Barabara wa Mamlaka ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini Johansen Kahatano amesema kuwa basi likiwa bovu halina na nafasi ya Kusafirisha abiria kwenda mikoani. Kahatano ameyasema hayo wakati alipokuwa katika ukaguzi wa mabasi katika kituo cha mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam. Amesema kuwa mabasi yote yaliyokuwa na kasoro askari wameyakagua na hawajaweza kufanya safari mpaka watakapotengeneza.

Amesema kuwa baadhi ya basi walipandisha nauli wameweza kuwabaini na wamewapiga faini ya shilingi 250,000. Kahatano amesema kuwa wamejipanga sawa katika kufanya  ukaguzi  katika cha mabasi Ubungo. Kwa upande wa Mwenyekiti wa Kutetea Abiria (Chakua) Hassan Mchachama amesema kuwa kazi ya Chakua ni  kutetea abiria kwa mjibu wa sheria. Amesema kuwa abiria akicheleweshwa ndani ya masaa mawili ya asubuhi kampuni husika inalazimika kuwanunua kifungua kinywa kwa abiria wote pamoja na kutafuta mbadala wa basi. Amesema Chakua ndio kimbilio la abiria katika kutafuta haki ya safari.
 Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Ibrahim Samwix akifanya kukaguzi katika basi katika kituo cha Ubungo jijini Dar es Salaam.
 Askari wa Kikosi cha  Usalama wa Barabarani waking'oa namba ya usajili katika basi baada ya kuwa na makosa mengi katika kituo cha mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.
Abiria wakiwa wameshuka katika basi walilokuwa wanasafiri na kupatiwa basi mbadala  na kampuni hiyo ni mara baada ya kuibanika na hitilafu nyingi katika ukuaguzi wa mabasi katika kituo mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad