HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, December 4, 2018

Ofisi ya Makamu wa Rais Kuwa Mfano Utunzaji Mazingira Mji wa Serikali

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. January Makamba akisalimiana na Mkurugenzi wa Mazingira toka Ofisi hiyo, Profesa. William Mwegoha alipotembelea eneo zinapojengwa Ofisi za Makamu wa Rais Muungano na Mazingira katika Mji wa Serikali Ihumwa jijini Dodoma leo tarehe 4, Desemba, 2018. Katikati ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Mhandisi Joseph Malongo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. January Makamba (katikati) akiteta jambo na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mussa Sima (kulia) na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Joseph Malongo wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya hatua za awali za ujenzi wa Ofisi za Makamu wa Rais zinazojengwa katika Mji wa Serikali Ihumwa jijini Dodoma leo tarehe 4, Desemba, 2018. 
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mhandisi Joseph Malongo akimuonyesha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. January Makamba (mwenyeshati ya njano) eneo lenye ukubwa wa ekari 8 katika Mji wa Serikali Ihumwa jijini Dodoma zinapojengwa Ofisi za Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira leo. Wapili kutoka kulia ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mussa Sima.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. January Makamba akielezea jambo alipokuwa akitazama mandhari ya eneo linalojengwa Ofisi za Makamu wa Rais alipofanya ziara katika eneo hilo lililopo Ihumwa jijini Dodoma leo.
Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira wakimskiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. January Makamba (hayupo pichani) wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya hatua za awali za ujenzi wa Ofisi za Makamu wa Rais zinazojengwa katika Mji wa Serikali Ihumwa jijini Dodoma leo tarehe 4, Desemba, 2018. 
Pichani kiwanja cha ukubwa wa ekari 8 ambacho panajengwa Ofisi za Makamu wa Rais Muungano na Mazingira kikiwa kimefanyiwa usafi tayari kwa kuanza ujenzi wa ofisi hizo. (Picha na: Frank Shija - MAELEZO, Dodoma)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad