HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, November 6, 2018

UONGOZI WA BENKI YA CRDB WAMTEMBELEA KATIBU MKUU WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James (kulia) akizungumza na Viongozi wa Benki ya CRDB waliofika ofisini kwake leo, kwa lengo la kumtambulisha Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Benki hiyo, Abdulmajid Nsekela (wa pili kushoto). Ujumbe wa Benki ya CRDB uliongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Ally Laay (kushoto), Naibu Mkurugenzi Mtendaji, Esther Kitoka pamoja na Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja, Tully Mwambapa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wa tatu kulia) akifafanua jambo wakati wa kikao chao na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James (kushoto) walipomtembela ofisini kwake, jijini Dar es salaam leo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James (wa pili kulia) akimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Ally Laay. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akijadiliana jambo na Naibu Mkurugenzi Mtendaji, Esther Kitoka wakati wa kikao chao na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James.
Picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad