HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, October 5, 2018

ALICHOKIFANYA DIAMOND TANDALE NI MFANO WA KUIGWA-MEYA SITTA

Na Khadija Seif, Globu ya jamii
MEYA wa Manispaa ya Kinondoni katika Jiji la Dar es Salaam Benjamin Sitta amesema msanii wa muziki wa kizazi kipya maarufu kwa jina la Bongo Fleva Nassib Abdull a.k.a Diamond ni mfano wa kuigwa katika jamii.

Sitta amesema Diamond ameona haja na umuhimu wa kurudisha shukrani kwa jamii na watu wa aina yake ni wachache sana.

Meya Sitta amesema hayo leo wakati sherehe iliyopewa jina la Ahsante Tandale ambapo Diamond ameamua kurejesha shukrani kwa wananchi wa maeneo hayo ambako yeye amezaliwa na kukulia.

Sitta amesema pamoja na mambo mengine uamuzi wa Diamond kutoa kadi za bima ya afya ambazo zitaweza kumpa nafasi kila aliyejiunga na huduma hiyo kupata matibabu bure kwa muda wa mwaka mmoja.

Wakati huo huo msaani Rashid Chid Benz amesema Diamond amefanya jambo kubwa na ni mfano ambao unastahili kuigwa na wasanii wote nchini.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta akizungumza wakati wa sherehe iliyopewa jina la Ahsante Tandale ambapo Diamond ameamua kurejesha shukrani kwa wananchi wa maeneo hayo ambako yeye amezaliwa na kukulia.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad