Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Taasisi ya Tulia Trust inayojihusisha na masuala ya Afya na Elimu nchini imeweza kuwasaidia watoto mbalimbali wanaoishi katika mazingira magumu na wengine kutoa fursa kwa vijana watano (5) kwenda kuendelea na elimu yao ya Sekondari Nchini Nigeria.
Tulia Trust ni shirika lisilo la kiserikali Trust lilianzishwa mwaka 2015 na Mheshimiwa. Dk. Tulia Ackson, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Balozi wa Tulia Trust Dotto Bernad Bwakeya ' Lameck Ditto" amesema kuwa katika kuchangia na kusaidia sekta ya Elimu Tulia Trust imetoa nafasi ya pekee kwa vijana watano (5) ambao watakwenda kuendelea na masomo ya sekondari Nchini Nigeria katika Taasisi ya Rochas Foundation College of Africa.
Ditto amesema Kupitia ziara mbalimbali za Dkt. Tulia katika Shule za Sekondari mkoani Mbeya alifanikiwa kukutana na kuunganishwa na vijana hao ambao wengi wao wanatoka katika hali duni kiuchumi, yatima na wengi wao wanalelewa na mzazi mmoja au ndugu.
Amesema jitihada zilizofanywa na Tulia Trust ni kuhakikisha vijana hawa ambao kielimu wamekua wakifanya vizuri achilia mbali changamoto walizonazo kiuchumi na waliweza kufaulu vizuri mitihani ya darasa la saba ni kuwapatia msaada wa kielimu kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
Taasisi ya Rocha Foundation imekuwa inashirikiana na taasisi mbalimbi barani Afrika ili kuwawezesha watoto wanaoishi katika mazingira magumu kupata nafasi ya kujiendeleza kielimu na tayari watoto wengine watano kutoka Dar es Salaam wameshapatikana nao wataelekea nchini Nigeria.
Nchini Nigeria Vijana hao Wataendelea na masomo mpaka kumaliza Elimu ya Sekondari, Tulia Trust itakua nao bega kwa bega mpaka wanahitimu Elimu zao za Sekondari , hii ni katika kuhakikisha wanapata Elimu bora.
Moja ya watoto hao Anne Bernad Shitindi ameishukuru Taasisi ya Tulia Trust kwa kuwapatia nafasi ya kwenda kujiendeleza kielimu nchini Nigeria na akiahidi kufanya vizuri katika masomo yako na kupeperusha vyema bendera ya Tanzania.
Mzee Lupyuto Mwamakula Ngubi ambaye ni Mlezi wa Mtoto Anna Bernad amewashukuru Tulia Trust kwa ufadhili huo wa Elimu kwa kijana wake ambaye alipoteza wazazi wake wote wawili akiwa bado mdogo. Amesema fursa hii itamsaidia Anna kupata Elimu nzuri na amemtaka yeye pamoja na wenzake wakasome kwa bidii.
Tulia Trusy imetoa nafasi hiyo kwa watoto wa kike wanne na wakiume mmoja ambapo Majina ya watoto ni hayo ni Anna Bernad Shitindi, Ayubu Andrea Mwaihola, Suzana Willy Mwakilima, Bernada Emmanuel Fuime, Beautiful Japhary Msinge na wataondoka alfajiri ya Ijumaa ya Agost 03 mwaka huu.
Balozi wa taasisi ya Tulia Trust, Dotto Bernad 'Ditto' akDitto'mza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar as Salaam, juu ya Taasisi ya Tulia Trust inavyolenga katika kuwasaidia watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu na kutoa fursa kwa vijana watano kwenda kusoma elimu ya sekondari nchi ya Nigeria.(Picha zote na Emmanuel Massaka Globu ya jamii)
Mlezi wa mtoto Anna Bernad, Mzee Lupyuto Mwamakula akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar as Salaam,ambapo ameishukuru Taasisi ya Tulia Trust kwa kumpeleka kijana wake kusoma nchi Nigeria.
Picha ya pamoja
No comments:
Post a Comment