HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, August 31, 2018

SHIRIKA LA POSTA TANZANIA LAELEZA MATARAJIO NA MALENGO YAKE KWA MWAKA 2018/2019

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Elia Madulesi, akizungumza wakati akiwakaribisha waandishi wa habari katika mkutano ambao Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika, Kanali Mstaafu, Dk. Haruni Kondo, alielezea mambo mbalimbali yanayohusu matarajio na malengo ya shirika hilo, kwa mwaka 2018/2019, jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Postamasta Mkuu, Hassan Mwang'ombe na kushoto ni Kaimu Meneja Mkuu Rasilimali za Shirika Macrice Mbodo.
Baadhi ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari, wakichukua taarifa iliyokuwa ikitolewa na  Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania, Kanali Mstaafu, Dk. Haruni Kondo. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Kanali Mstaafu, Dk. Haruni Kondo, akizungumza na waandishi wa habari, wakati alipokuwa akielezea masuala mbalimbali yanayohusu matarajio na malengo ya shirika hilo, kwa mwaka 2018/2019. Kushoto ni Postamasta Mkuu wa shirika, Hassan Mwang’ombe.  
Baadhi ya wapiga picha na waandishi wa habari, wakichukua taarifa kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta, Kanali Mstaafu, Dk. Haruni Kondo.
Baadhi ya wapiga waandishi wa habari, wakisikiliza taarifa  iliyokuwa ikitolewa na Mwenyekiti wa Bodi, Kanali Mstaafu, Dk. Haruni Kondo. 
Mwenyekiti wa Bodi, Kanali Mstaafu, Dk. Haruni Kondo (katikati), akizungumza na waandishi katika mkutano huo.  
Postamasta Mkuu, Hassan Mwang'ombe, akizungumza katika mkutano huo, wakati alipoelezea kuhusu duka la Shirika la kwenye mtandao kwamba sasa tayari linafanya kazi na kuwataka wananchi kulitumia kwa kuweka bidhaa zao ili kuweza kuuza ndani na nje ya nchi. Kulia Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika, Kanali Mstaafu, Dk. Haruni Kondo.
Maofisa wa Kitengo cha Mawasiliano cha Shirika la Posta Tanzania (TPC),wakiwa katika mkutano huo, wakimsikiliza Postamasta Mkuu wa shirika hilo, Hassan Mwang'ombe, alipokuwa akizungumza katika mkutano huo, jijini Dar es Salaam leo. 
Postamasta Mkuu, Hassan Mwang'ombe,akizungumza wakati alipokuwa akijibu maswali yaliyokuwa yakiulizwa na waandishi wa habari katika mkutano huo,jijini Dar es Salaam leo.   
Mwenyekiti wa Bodi, Kanali Mstaafu, Dk. Haruni Kondo akijibu maswali yaliyokuwa yakiulizwa na waandishi wa habari katika mkutano huo.   

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad