HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, August 9, 2018

NAIBU WAZIRI MGALU AMUAGIZA DC SUMBAWANGA KUTUMIA MAMLAKA YAKE KUWATUPA NDANI SAA 48 WASIMAMIZI WA UTEKELEZAJI WA MRADI WA REA


 Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akihutubia wananchi wa kata ya Mtowisa wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa, leo akiwa katika ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya REA awamu ya tatu. (0163 -205, 207)
 Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akiwahoji maswali wasimamizi kutoka kampuni ya kampuni ya Nakuroi Investment inayosuasua katika utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa REA awamu ya tatu katika vijiji vya mkoa wa Rukwa, leo mbele ya wananchi wa kata Mtowisa, Sumbawanga mkoani Rukwa. (0179 - 80)
 Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akitoa ufafanuzi wa jambo kwa msimamizi wa kampuni ya Nakuroi Investment kuhusu ujenzi wa miundombinu ya usambazaji wa umeme katika kijiji cha Kilyamatundu wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa, ambapo yupo katika ziara ya kikazi mkoani humo. (417)
 Baadhi ya watumishi wa Shirika la umeme nchini, Tanesco mkoawa Rukwa wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri Subira Mgalu wakati aliwahutubia wananchi wa kata ya Mtowisa mkoani Rukwa leo, ambapo yupo katika ziara ya kikazi ya kukaguautekelezaji wa miradi ya REA awamu ya tatu.(0150)

Na Mwandishi wetu, Rukwa.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amemuagiza Mkuu wa wilaya ya Sumbawanga, Dk. Halfan Haule kutumia mamlaka yake kuwatupa ndani saa 48 wasimamizi wa utekelezaji wa mradi wa usambazaji umeme vijijini (REA) awamu ya tatu wa Kampuni ya Nakuroi Investment iwapo watasuasua katika ujenzi wa miundombinu ya umeme wilayani humo.

Naibu Waziri huyo, ametoa agizo hilo leo akiwa katika kijiji cha Kilyamatundu kilichopo mpakani mwa mikoa ya Mbeya na Songwe tarafa ya Kipeta wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi inayolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya REA awamu ya tatu mkoani humo.

Kabla ya kuoa agizo hilo, Naibu Waziri huyo alionyeshwa miundombinu inayowezesha upatikanaji wa umeme katika kijiji jirani cha Kamsamba iliyopo umbali wa mita 100 na kuonyesha kushangazwa kwanini Kijiji cha Kilyamatundu kinashindwa kunufaika na huduma ya umeme kwa kuwa miundombinu ipo jirani kiasi hicho.

"Mkandarasi nataka nguzo na vifaa vingine vifike hapa Alhamisi ijayo kama ulivyoahadi na ujenzi wa miundombinu ya umeme ianze mara moja,.......mkuu wa wilaya hakikisha inatumia mamlaka yako kuwatupa ndani saa 48 hawa jamaa kama watasuasua kutekeleza mradi huu, sisi lengo letu umeme upatikane hapa kijijini haraka iwezekanavyo" alisema

Aliongeza kwamba hatua hizi zichukuliwe kwa kuwa kampuni hii imekuwa ikishindwa kutekeleza mradi huu kwa wakati, hivyo kuonyesha dalili ya kushindwa kumaliza kwa muda uliopangwa.

Kwa upande wake, mkuu wa wilaya hiyo Dk. Haule aliahidi kutekeleza agizo hilo kwa kuwa serikali imechoka kuendelea kuchonganishwa na wananchi kwa uzembe wa baadhi ya watu hivyo sheria lazima ichukue mkondo wake.

Aidha, Mbunge wa jimbo hilo Iginas Malocha alisema kuwa iwapo eneo hilo litapata huduma ya umeme ni wazi kwamba thamani ya mazao yao kama vile mpunga itaongezeka na wakulima kuwa na uhakika wa soko.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad