HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, June 14, 2018

WANAFUNZI WA CHUO CHA SAUT MWANZA WATEMBELEA ENEO LA MAKABURI YA HISTORIA YA MAUAJI YA KIMBARI RWANDA


 Mwanafunzi wa chuo cha mtakatifu Augustino katisali mbele ya Moja la kaburi la pamoja la wahanga wa mauaji ya Kimbari Kigari nchini Rwanda.


WANAFUNZI wa chuo cha Mtakatifu Augustino cha jijini Mwanza(SAUT) wa mwaka wa kwanza na wapili wanaosoma kozi ya mawasiliano ya umma watembelea kituo cha kumbukumbu na Makaburi ya halaiki ya wahanga wa mauaji ya Kimbari Kigali nchini Rwanda.



Kituo hicho ambacho kimebeba historia ya nchi ya Rwanda pamoja na baadhi kumbukumbu ya vitu mbalimbali vya watu wa nchi ya Rwanda kabla na baada ya mauaji ya kimbari.


Baadhi Kumbukumbu zilizopo katika jengo la kumbukumbu ni picha za watu waliofariki dunia pamoja na picha za watoto ambao waliuwawa bila hatia yoyote mauaji na makaburi yalitokea Aprili 7, 1994.


Pia katika ziara hiyo wanafunzi wa chuo cha MT. Augustino walitembelea televisheni ya Taifa ya Rwanda, Rwanda Bordicasting Agency (RBA) na kujifunza vitu mbalimbali katika shirika hilo la utangazaji nchini Rwanda.

Lango la kuingilia katika makumbusho na Makaburi ya mauji ya kimbari Kigari nchini Rwanda. Baadhi ya Wananfunzi wa chuo cha Mtakatifu Augustino Mwanza wakiingia katika eneo la kumbukumbu.
 Mmoja wa wafanyakazi wa kituo cha kumbukumbu ya makaburi ya mauaji ya kimbari, Kazinimana Pacifique akizungumza na wanafunzi wa chuo kikuu cha MT Augustino jijini Mwanza mara baada ya kufika katika kituo cha kumbukumbu na makaburi ya pamoja ya mauaji ya Kimbari ambayo walitokea nchini Rwanda Mwaka 1994 ambapo mpaka kwaka huu 2018 wametimiza miaka 24 ya kumbukumbu ya mauaji hayo.Kushoto ni Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano wa Chuo cha Mtakatifu Augustino(HOD), Peter Mwidima.

 Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano wa Chuo cha Mtakatifu Augustino(HOD), Peter Mwidima akizungumza na wanafunzi wa  huo cha mtakatifu Augustino jijini Mwanza walipowasili katika kituo cha makaburi ya haraiki ya mauaji ya Kimbari Kigari nchini Rwanda.
 Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha Mtakatifu Austine wakiingia  katika chumba cha kuangalia moja ya sinema.
  Baadhi ya wanafunzi wanafunzi wakipiga picha nje ya Jengo ambalo limebeba historia ya nchi ya Rwanda pamoja na picha za wahanga wa mauaji ya kimbari na vitu mbalimbali ambavyo vimehifadhiwa humo.

 Baadhi ya wanafunzi wakiwa katika eneo ambapo kunamajina ya watu waliofariki dunia katika mauaji ya kimbali Nchini Rwanda.


Baadhi ya Majina ya watu waliouwakawa wakati wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda
 Baadhi ya wanafunzi wa Chuo cha Mtakatifu Augustino jijini wanza wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya Kiislam ya nchini Rwanda mara baada ya kukutana katika makumbusho na makaburi ya mauaji kimbari.
 Jengo la ukumbi Mkuu wa Ktituo cha utoaji huduma kwa pamoja Rusumo ambalo lipo mpakani mwa Tanzania na Rwanda.
 Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha Mtakatifu Augustino cha jijini Mwanza wakipanda gari maara baada ya kufika mpakani mwa Tanzania na Rwanda. 
Wanafunzi wa chuo cha Mt. Augustino jijini Mwanza wakiwa katika picha ya pamoja na Mhariri mkuu Mtendaji wa Kituo cha Utangazaji cha Rwanda Broadcasting Agency. na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha chuo cha Mtakatifu Augustino,(HOD), Peter Mwidima. 
 Jengo la Kituo cha Utangazaji cha Rwanda Broadcasting Agency nchini Rwanda ambapo kuna kituo Vituo vya Redio mbalimbali pamoja na Televisheni ya Taifa ya Rwanda(RBA).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad